Saturday 24 June 2017

Serikali, TOC wakutana Dodoma kujadili maandalizi Michezo ya Jumuiya ya Madola 2018

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe (wa pili kulia) na Naibu wake, Anastazia Wambura (kulia),  Makamu wa Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Henry Tandau (kushoto) na  Katibu Mkuu Filbert Bayi waliokutana mjini Dodoma juzi.
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI na Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) zimekutana na kujadili kwa kina kuhusu maandalizi ya Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Gold Coast, Australia kuanzia Aprili.

Michezo ya 21 ya Jumuiya ya Madola itafanyika Gold Goast kuanzia Aprili 4 hadi 15, mwakani, ambapo Tanzania itakuwa miongoni mwa nchi zitakazoshiriki michezo hiyo.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe na naibu wake, Anastazia Wambura juzi mjini Dodoma walikutana na Makamu a Rais na  Katibu Mkuu wa TOC, Henry Tandau na Filbert Bayi, ambao walijadili kwa kina maandalizi ya Tanzania kwa ajili ya michezo hiyo.

Bayi alisema kuwa majadiliano yao yalienda vizuri, ambapo waliueleza ujumbe huo wa Serikali kuhusu mpango wa maandalizi wa Diplomasia ya Michezo, ambao ungeziwezesha timu za Tanzania za riadha, kuogelea, ngumi na mpira wa meza kupiga kambi nje ya nchi kwa ajili ya maandalizi hayo.

Alisema tofauti na mwaka 2014 wakati wa maandalizi ya Michezo ya Jumuiya ya Madola iliyofanyika Glasgow, Scotland, Serikali iligharamia nauli na posho za wachezaji walioenda katika kambi katika nchi za  Uturuki, Ethiopia, China na New Zealand kwa kutumia mpango wa Diplomasia ya Michezo.

 Bayi alisema TOC mwaka huu ndio itagharamia nauli na posho kwa wachezaji na makocha watakaoenda kuiga kambi nje ya nchi kwa ajili ya kujiandaa na Michezo ya Jumuiya ya Madola ya Gold Coast mwakani.

Alisema Mwakyembe ambauye aliingia hivi karibuni katika wizara hiyo akichukua nafasi ya Nape Nnauye aliyeondolewa na Rais Magufuli, alikua hana taarifa kuhusu mpango huo wakati TOC ilishasilisha suala hilo maema wakati wa Nape.

Alisema Mwakyembe aliahidi kulifanyia kazi suala hilo na TOC wana mpango wa kukutana na Waziri wa Mambio ya Nchi za Nje, Augustino Maige, ili kuhakikisha timu ya Tanzania inapiga kambo haraka nje ya nchi kwa ajili ya maandalizi ya michezo hiyo.


Tanzania katika michezo hiyo ya Gold Coast inatarajia kupeleka timu za riadha, ngumi na mpira wa meza, ambazo zinatarajia kupiga kambi Ethiopia, Cuba na China.

No comments:

Post a Comment