Tuesday 27 June 2017

Ngoma azichezesha ngoma Yanga, Simba

Na Mwandishi Wetu
MSHAMBULIAJI wa Kimataifa wa Zimbabwe, Donald Ngoma amezikacha klabu za Yanga na Simba na badala yake amemwaga wino timu ya Polokwane City inayoshiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini, imebainika.

Ngoma anatarajia kutua jijini Dar es Salaam kesho kwa ajili ya kuongeza mkataba wa kuendelea kuichezea Yanga, lakini pia mshambuliaji huyo alishafanya mazungumzo ya awali na viongozi wa Simba na inasemekana ujio wake ulikuwa ni kwa  ajili ya kukamilisha usajili wake kwa kusaini mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo msimu ujao.

Kwa mujibu wa Mtandao wa KickOff.com, Ngoma raia wa Zimabwe, amekamilisha zoezi lake la usajili kwenye klabu hiyo, baada ya kuwa huru kufuatia kumaliza mkataba wake wa miaka miwili na mabingwa wa soka Tanzania Yanga.

Taarifa hiyo imesema Ngoma,  alisaini mkataba huo wa miaka mitatu baada ya kufuzu vipimo vya afya na anatarajiwa kujiunga na miamba hao wa ligi ya ABSA,ambao kwasasa wanashika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi hiyo.


Akiwa Polokwane City, Ngoma anatarajiwa kukutana na Mzimbabwe mwezake, George Chigova aliyewahi kucheza naye FC Platinum chini ya kocha Norman Mapeza.

No comments:

Post a Comment