Tuesday 20 June 2017

Gaidi auawa akitaka kulipua steshen Ubelgiji

BRUSSELS, Ubelgiji
ASKARI wa Ubelgiji wamempiga risasi na kumuua mtu mmoja anayedai kuwa alikuwa akitaka kulipua stesheni ya treni mjini hapa, imeelezwa.

Mtu huyo aliuawa mara baada ya kuripotiwa kuwa alikuwa akiunganisha vilipuzi na hakuna mtu mwingine aliyejeruhiwa katika tukio hilo.

Waendesha mashtaka walisema kuwa mtu huyo alikufa. Wanalichukulia tukio hilo kama shambulio la kigaidi.

Machi mwaka 2016, watu 32 waliuawa katika shambulio la kigaidi mjini hapa, tukio mabalo lilidai kutekelezwa na kundi la kigaidi la Islamic State (IS).

Kwa mujibu wa gazeti la Ubelgiji la La Libre Belgique, liliwakariri waendesha mashtaka, mtu aliyeuawa alikuwa amevalia vilipuzi.

Nicolas Van Herrewegen, wakala wa relwe, alisema alikwenda chini katika stesheni, ambako alisikia mtu akipiga kelele.

"Baadae alikuwa akisema 'Allahu Akbar' na alitupa sanduku lake la matairi, “aliliambia Shirika la habari la AFP.

"Nilikuwa nyuma ya ukuta wakati mlipuko mdogo ukitokea. Nilikwenda chini na kuwataarifu wenzangu. Mtuhumiwa aliendelea kuwepo eneo hilo na baadae hatukumuona tena.”

"Haukuwa mlipuko mkubwa lakini kishindo chake kilikuwa kizito, “aliongeza. “Watu walikimbia huku na huko.”

Bwana Van Herrewegen akimuelezea muhusika huyo alisema alikuwa mtu mwenye mwili uliojengeka akiwa na nywele fupi, akiwa amevali shati jeupe na suruali ya jinsi.

"Niliona kama alikuwa na kitu fulani niliona waya, huenda alikuwa amevalia vesti yenye vilipuzi, “alisema.

Mwanasheria Remy Bonnaffe, 23, alikuwa akisubiri treni alifanikiwa kupiga picha ya moto huo mdogo baada ya mlipuko.

Aliliambia Shirika la Habari la Reuters kuwa watu waliokuwa karibu na mlipuko huo hawakuumia na hakuna ukuta ulioharibika.

"Nina furaha kuwa hakuna mtu aliyeumia nan i wazi kuwa jaribio hilo halijafanikiwa, limefeli, “alisema.


Arash Aazami ambaye aliwasili muda mfupi katika stesheni hiyo baada ya mlipuko huo, alisema alikuta watu wa usalama, huku watu wengine wakikimbia mitaani kusaka usalama…, “alisema.

No comments:

Post a Comment