Saturday 30 December 2017

Yanga Yatamba Kuipasua Mbao FC Mwanza

Na Mwandishi Wetu, Mwanza
KOCHA msaidizi wa timu ya soka ya Yanga, Shadrack Nsajigwa ameahidi ushindi katika mchezo wao wa kesho wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mbao FC utakaochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mkoani hapa.

Akizungumza katika mazoezi ya klabu hiyo katika uwanja huo, Nsajigwa alisema timu yake ipo katika hali nzuri na wachezaji wake wote ni wazima.

"Tumefanya mazoezi leo(jana Jumamosi) na tutapambana kuhakikisha tunashinda,wachezaji wote tuliokuja nao wapo katika hali nzuri.Hatuna hofu tumeanda timu kwajili ya ushindi," alisema Nsajigwa.

Akielezea kuhusu wapinzani wake,Nsajigwa alisema Mbao FC ni timu nzuri na ina wachezaji wanaopambana muda wote.

Nsajigwa alisema anawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi ili kuhakikisha wanaishangilia timu yao.

Katika msimamo wa Ligi Kuu, Yanga wapo katika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 23 baada ya michezo 11.

Yanga imeshinda mechi Sita na kutoka sare mechi tano.Yanga imefungwa mabao matano na kufunga mabao 17.Mbao FC wapo katika nafasi ya nane wakiwa na alama 11.


Mbao FC wameshinda mechi mbili na kutoka sare mechi tano.Timu hiyo imepoteza mechi nne  na imefungwa mabao 13 huku yenyewe imefungwa mabao 11.

No comments:

Post a Comment