Friday 8 December 2017

Guardiola Hafikirii kuvunja rekodi kwa sasa


MANCHESTER, England

KOCHA wa Manchester City Pep Guardiola anasema kuwa nafasi ya kueka historia haiku katika mawazo yake wakati anajiandaa kwa derby ya Jumapili dhidi ya wapinzani wao wakubwa Manchester United.

Endapo Man City atashinda mchezo huo utakuwa huo ni ushindi wao wa 14 mfululizo wa ligi, ukiwa ni rekodi kwa timu kushinda idadi hiyo ya mechi katika msimu mmoja wa Ligi Kuu.

Hatahivyo, Guardiola anasema kuwa kwa sasa anaangali jinsi atakavyopanga mipango yake kuhakikisha anakifunga kikosi cha kocha Jose Mourinho.

"Rekodi itaunjwa, lakini nachoangalia ni jinsi gani tutashida mchezo huo, alisema.

"Ikiwa unacheza mchezo mmoja alafu unafikiria kuhusu rekodi basi utasahau nini unachotakiwa kufanya.

NANI ATASHINDA MCHEZO?

Hii ni derby ya kwanza tangu Aprili mwaka 2013 ambako klabu hizo mbili zilipokutana wakati zikishikilia nafasi mbili za kwanza katika msimamo.

Endapo Man City itashinda kwenye Uwanja wa Old Trafford watakaa pointi 11 zaidi ya United ambao watapunguza hadi kubaki pointi tano, endapo watashinda mchezo huo.

Guardiola anaamini kuwa ni mapema mno kuamua nani atashinda ,chezo huo.

"Kushinda, kutoka sare au kushindwa Jumapili, hatuendi kushindwa au kushinda Ligi Kuu. Ni Desemba, alisema.


"Kuna pointi nyingi za kuzitafuta, zaidi ya 70, Kwa sasa tunaangalia mchezo huo.

No comments:

Post a Comment