Sunday 10 December 2017

Mr Tanzania 2017 kupatikana Desemba 15 MayFair

Mwenyekiti wa Kamati ya Shindano la Mr Tanzania 2017, Nilesh Bett akizungumza na wanahabari kuhusu shindano hilo. Kushoto ni Katibu wa Shirikisho la Mchezo wa Kutunisha Misuli Tanzania (TBBF), Francis Mapugilo.
Na Mwandishi Wetu
SHINDANO la kumsaka MR Tanzania 2017 litafanyika jijini Dar es Salaam Desemba 15 katika hoteli ya MayFair, imeelezwa.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kujenga Mwili Tanzania (TBBF), Francis Mapugilo alisema jijini Dar es Salaam kuwa, maandalizi ya shindano hilo yanaendelea vizuri na hadi sasa kuna washiriki 60, ambao watachujwa na kubaki 30 watakaoingia kambini.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kunyanyua Vitu Vizito Tanzania, TBBF, Francis Mapugilo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu shindano la Mr Tanzania 2017 litakalofanyika Desemba 13, 2017. Kulia ni msemaji wa Pilipili Entertainment, Mzee Chilo na kushoto ni mwenyekiti cha TBBF,, Nemes Chiwalala.
Akifafanua kuhusu kumpata Mr Tanzania 2017, Mapugilo alisema kuwa Desemba 12 kutakuwa na shindano la kumsaka Fashion Icon, ambalo litafanyika kwa Hussein Pamba Kali, ambalo washiriki watavaa nguo mbalimbali na yule mwenye mwonekano mzuri atashinda.

Alisema siku inayofuata, kutakuwa na shindano la kumsaka Mr Fit, ambapo washiriki watachuana katika mazoezi mbalimbali yakiwemo kuchomoka kwa kasi, kupiga pushapu na mazoezi mengine.
Mapugilo alisema kuwa shindano jingine dogo litafanyika Desemba 14, ambalo litakuwa kumsaka Mr Photojenic, ambalo litafanyikia katika eneo la kuogelea la hoteli ya MayFair.

Alisema katika shindano hilo atatafutwa mshiriki mwenye m uonekano mzuri katika picha, ambapo pia washiriki watatembea na kupozi ili kupata picha nzuri,ambazo zitashindanishwa na kumpata mshindi.

Alisema yote hayo yatakamilishwa Desemba 15 kwa shindano kubwa na mshiriki atakayekuwa maarufu zaidi ndiye atayeibuka Mr Tanzania 2017 na kupata nafasi ya kushiriki mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Naye Mwenyekiti wa Shindano hilo, Nilesh Batt alisema kuwa shindano hilo limeandaliwa vizuri  ili kuhakikisha mshindi wa ukweli anapatikana ambaye atawakilisha vizuri Tanzania katika mashindano ya kimataifa ya Mr Afrika pamoja na yale ya dunia yatakayofanyika mwakani Nigeria na Uingereza.

No comments:

Post a Comment