Friday 29 December 2017

Wenger anyoosha mikono kwa Sanchez

LONDON, England
KOCHA Arsene Wenger anasema kuwa hawezi kumuhakikishia mshambuliaji Alexis Sanchez (pichani) kubaki Arsenal kwa muda mrefu, baada ya mshambuliaji huyo kufunga mara mbili walipocheza jana dhidi ya Crystal Palace.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Chile anaweza kuondoka kama mchezaji huru katika kipindi cha majira ya joto wakati mkataba wake utakapomalizika na amekuwa akihusishwa na kutaka kuhamia kwa vinara wa Ligi Kuu ya England Manchester City, ambao walishindwa kukamilisha usajili wa mchezaji huyo siku a mwisho ya usajili.

Alipoulizwa kuhusu hatma ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 2, kocha huyo Mfaransa alisema: "Hakuna mtu hajuae nini kitatokea. Kwa kweli ni vigumu sana kutabiri.

"Kwa sasa tunaangalia mambo ya muda mfupi, hiyo ikiwa na maana mchezo ujao na wachezaji waliojituma na ambao wako tayari kupambana. Haina uhakika utakuwe;po mahali Fulani kwa muda gani.

"Wakati wote wanahoji, wakati watu hawana mikataba ya muda mrefu, Njia bora ya kuonesha jinsi watu walivyojituma ni jinsi watakavyoonesha kiwango chao uwanjani.”

Maoni yake hayo yamekuja mwezi mmoja baada ya kuzungumza kuhusu wachezaji wote wawili, Sanchez na kiungo Mjerumani Mesut Ozil, ambao mikataba yao ya sasa inamalizika katika kipindi cha majira ya joto, akitaka wabaki kwenye Uwanja wa Emirates.


Jana Alhamisi, Sanchez alifunga mara mbili katika dakika nne wakati Arsenal ikiibuka na ushindi baada ya ndros Townsend akifuta bao la kuongoza la Shkodran Mustafi.

No comments:

Post a Comment