Friday 8 December 2017

Mkutano Mkuu wa Kawata wafunguliwa Zanzibar


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
WACHEZAJI wametakiwa kuongeza jitihada katika mazoezi ili kupata nafasi ya ushiriki Michezo ya Olimpiki na kupata sifa ya kuwemo katika Kamisheni ya Wachezaji Tanzania (Kawata), imeelezwa.

Hayo yalielezwa jana mjini hapa na Makamu wa Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Henry Tandau wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Kawata katika ukumbi wa mikutano wa Amani, Welezo.

Makamu wa Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Henry Tandau na Katibu wa Kamisheni ya Michezo Tanzania (Kawata), Amina Ahmed.
Tandau ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) alisema kuwa, idadi ya wajumbe wa Kawata itapungua baada ya wajumbe wengi kukosa sifa, kwani wanaotakiwa ni wale tu walioshiriki Michezo ya Olimpiki.

Kawata ilikuwa inaundwa na wachezaji hai kutoka vyama au mashirikisho mbalimbali ya michezo nchini, bila kujali kama wameshiriki Olimpiki au la.
Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi akizungumza katika mkutano Mkuu wa Kawata Zanzibar leo.
Tandau alisema kuwa wamepokea walaka kutoka Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC) unaoagiza kuwa kuanzia sasa wajumbe wa kamati za wachezaji ni wale tu watakaokuwa wameshiriki Olimpiki.

Alisema mjumbe atakuwa halali kwa vipindi itatu tangu alliposhiriki Olimpiki ya mwisho na baada ya hapo atastaafu kuwa mjumbe wa kamati hiyo.

“Hii ya mjumbe kuwa halali baada ya Olimpiki tatu tangu aliposhiriki ile ya mwisho ilikuwepo, lakini kipya ni lazima mjumbe wa Kawata awe ameshiriki Michezo ya Olimpiki, “alisema Tandau.

Alpoulizwa baada ya mkutano huo kutokana na walaka huo haoni kuwa wajumbe wa Kawata watapungua sana kwa kuwa vyama ingi vimeshindwa kupeleka wachezaji katika Olimpiki, Tandau alikiri hilo na kuwataka kufanya jitihada ili kushiriki michezo hiyo.

Wakati huohuo,  Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi alisema wamesikitishwa na kitendo cha baadhi ya vyama vya michezo kushindwa kuleta wajumbe katika mkutano huo wa Kawata licha ya kugharamia kila kitu.
Baadhi ya wajumbe wa Kawata katika mkutano mkuu leo Zanzibar.
Baadhi ya vyama hivyo ni Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) na vingine.




No comments:

Post a Comment