Monday 25 December 2017

Kifimbo cha Malkia chatua Brisbane, Australia

Mbio za Kifimbo cha Malkia wa Uingereza zilianza Machi 13 mwaka huu.

BRISBANE, Australia

BAADA ya kuanza safari yake kutoka Buckingham Palace Machi 13 mwaka huu jijini London, Kifimbo cha Malkia hatimaye kimewasili kwa waandaaji wa Michezo ya Jumuiya ya Madola nchini Australia leo na sasa kinaelekea katika mji wa Gold Coast.

Kifimbo hicho kiliwasili jijini hapa asubuhi ya leo baada ya kusafiri kwa takribani siku 288 na kutembelea mataifa yote ya Jumuiya ya Madola.

Leo ambayo ni siku ya Krismas inabakisha siku 100 kamili kabla ya kuanza kwa michezo hiyo ya 21 tangu kuanza kufanyika kwake.

Balozi wa Gold Coast 2018 na muogeleaji Mcameroon McEvoy alipokea kifimbo hicho kutoka kwa Hugh Graham, ambaye ni makamu wa rais wa Shirikisho la Michezo ya Jumuiya ya Madola kwa Kanda ya Oceania, kufuatia kuwasili kutoka New Zealand.


Umati mkubwa wa watu akiwemo Borobi, walikusanyika kumuona McEvoy akibeba Kifimbo katika ukumbi wa Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Brisbane, asubuhi ya pilika pilika nyingi katika mwaka.

No comments:

Post a Comment