Friday 15 December 2017

Taifa Cup Netiboli Kuanza Rasmi Jumapili Arusha

Na Mwandishi Wetu
KINYANGANYIRO cha kumsaka bingwa wa taifa wa netiboli Tanzania kinaanza rasmi Jumapili kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha na Katibu Tawala wa Mkoa huo, Richard Kwitega ndiye anatarajia kuwa geni rasmi katika ufunguzi huo.

Katibu Mkuu wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta), Judith Ilunda amesema kuwa, ufunguzi rasmi utafanyika Jumapili na timu za mikoa ya Morogoro na wenyeji Arusha ndio itafungua mashindano hayo.

Ilunda amesema kuwa mechi ya pili Jumapili ni ile itakayozikutanisha timu za mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro, ambay ndio italayofunda dimba siku hiyo.

Amesema kuwa mechi za mashindano hayo zinatazamiwa kuanza Jumamosi kabla ya ufungizi rasmi Jumapili, ambapo kutakuwa ne mpambano kati ya Kigoma watakaocheza dhidi ya Arusha kuanzia saa 8:00 mchana, huku mkoa wa Songwe ukitoana jasho na Kigamboni kabla ya Morogoro haijapepetana na Kagera.

Ilunda anasema kuwa hadi sasa jumla ya mikoa 12 ilikuwa imethibiisha kushiriki mashindano hayo yanayotarajia kumalizika Desemba 23 mwaka huu, ambapo washindi watakabidhiwa zawadi zao vikiwemo vikombe na vyeti vya ushiriki.

Anasema kuwa uongozi wake ambao uliingia madarakani Septemba 30 mjini Dodoma, unaendesha mashindano kwa shinda kutokana na ukosefu wa fedha nan i matumaini yao kuwa wadau wa netiboli ikiwemo Serikali itawasaidia kufanikisha majukumu yao.

Awali, mashindano hayo yalipangwa kuanza Desemba 10, lakini yaliahirishwa kutokana na Chaneta kushindwa kupata zaidi y ash milioni 20 kwa ajili ya kuendeshea mashindano hayo ya Taifa Cup.


Hivi karibui Chaneta iliendesha kwa mafanikio makubwa mashindano ya Ligi Daraja la Pili Taifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam, ambapo timu saba zilipanda daraja.

No comments:

Post a Comment