Saturday 9 December 2017

Ukata wakwamisha kufanyika Taifa Cup ya netiboli

Na Mandishi Wetu, Zanzibar
MASHINDANO ya Kombe la Taifa ya netiboli yaliyopangwa kuanza kesho mjini Arusha, yameahirishwa kwa sababu ya ukata, imeelezwa.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta) Judith Ilunda, amesema leo kwa njia ya simu kutoka jijini Dar es Salaam kuwa, mashindano hayo sasa yatafanyika kuanzia Desemba 16 hadi 23 mjini Arusha.

Alisma awali mashindano hayo yangeanza Desemba 10 hadi Desemba 19 na sasa baada ya kuahirishwa yatamalizika Desemba 23 kenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Ilunda alisema kuwa chama chake kinahitaji kiasi cha sh milioni 29 kwa ajili ya kuendeshea mashindano hayo, ambayo hushirikisha timu za mikoa.

Alisema tayari wamepiga hodo kwa wadau mbalimbali wakiomba wawasaidie kupatikana kwa fedha hizo ili waweze kufanikisha mashindano hayo muhimu.

Alisema kuwa Chaneta inakabiliwa na ukata licha ya uongozi huo mpya kukutana majukumu mengi tangu uiongie madarakani miezi michache iliyopita mjini Dodoma.

Chaneta ilipoingia madarakani imeendesha kwa mafanikio mashindano ya Ligi Daraja la Kwanza yaliyofanyika kwenye viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam na timu saba kupanda daraja.


No comments:

Post a Comment