Monday 25 December 2017

Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania yakutana JNIA katika kikao cha kawaida


 Bodi ya Ushauri (MAB) ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) katika kikao cha kawaida cha 33 cha kujadili masuala mbalimbali ya utendaji ya mamlaka kwa kipindi cha robo ya kwanza na pili ya mwaka wa fedha 2017/2018.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (kulia) akimweleza jambo Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri (MAB) ya mamlaka hiyo, Prof. Mhandisi Ninatubu Lema (katikati),  katika kikao cha 33 cha Kawaida cha kujadili robo ya kwanza na pili ya mwaka wa fedha 2017/2018 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

Wajumbe wa Bodi ya Ushauri (MAB) ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, wakiwa katika kikao cha kawaida cha 33 cha kujadili masuala mbalimbali ya utendaji kwa kipindi cha robo ya kwanza na pili ya mwaka wa fedha 2017/2018 kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

Mjumbe wa Bodi ya Ushauri (MAB) ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, Dr. Frederick Mwakibinga (kushoto) akizungumza jambo kwenye kikao cha 33 cha bodi hiyo cha kujadili robo ya kwanza na pili ya mwaka wa fedha 2017/2018, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA). 

No comments:

Post a Comment