Tuesday 19 December 2017

Real Ikifungwa na Barcelona ndio basi tena La Liga


MADRID, Hispania
KLABU ya Real Madrid endapo itafungwa katika mchzo wao wa El Classico dhidi ya Barcelona, basi itakuwa imetupwa nje ya mbio za kusaka ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania ya La Liga kagika mchezo utakaofanyika wikiendi hii.
Endapo itashinda, na ikifuatiwa na ushindi mwingine  kutaiwezesha timu hiyo kupunguza tofauti ya pointi dhidi ya Barcelona na kuwa  pointi tano kabla ya mapumziko ya kipindi cha baridi na kukipa kikosi cha  Zinedine Zidane nafasi ya kupambana.
Mpambano huo wa El Clasico kwa timu hizo kupambana katika mpmbano wa La Liga ni wa kwanza tangu Aprili.
Tangu walipofugwa na Real Madrid katika mchezo wa Supercopa de Espana katika kipindi cha majira ya joto. Barca wametamba zaidi dhidi ya wapinzani wao.

TAARIFA ZA TIMU
Rais wa Real Madrid, Florentino Perez anatazamia Gareth Bale atacheza kufuatia kufanya vvizuri katika Kombe la Klabu Duniani.

Na Cristiano Ronaldo anataka Bale kucheza katika nafasi ya Isco kutokana na kutoelewana na Muhispania huyo wa Kimataifa.

Majeruhi Paco Alcacer hatakueemo katika kikosi cha Barcelona licha ya kufanya kazi nzuri msimu huu katika klabu hiyo, baada ya kufunga mabao yote katika ushindi wa timu hiyo wa mabao 2-1 nyumbani dhidi ya Sevilla.

HISTORIA YA MECHI ZAO

Mchezo huo wa Jumapili utakuwa ni wa 236 wa kiushindani kukutana timu hizo zenye upinzani wa hali ya juu katika soka.

No comments:

Post a Comment