Monday 11 December 2017

Chelsea, Real mtihani mgumu 16 bora Ulaya

Real Madrid
ZURICH, Uswisi
KLABU ya Chelsea itakuwa na mtihani mgumu kutinga robo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kupangwa kucheza dhidi ya Barcelona katika mchezo wa hatua ya 16 bora,  wakati Tottenham itakabiliana na mabingwa wa Italia Juventus katika mchezo mwingine wa hatua hiyo.

Vinara wa Ligi Kuu ya England Manchester City wenyewe watakabiliana na wawakilishi wa Uswisi Basel, Manchester United wenyewe watacheza dhidi ya timu inayoshiriki Ligi Kuu ya Hispania, La Liga ya Sevilla na Liverpool watatoana jasho dhidi ya timu ya Ureno ya Porto.

Mabingwa watetezi wa Kombe la Ligi ya Mabingwa wa Afrika Real Madrid wenyewe watakabiliana na vinara wa Ufaransa Paris St-Germain.

England imeweka rekodi kwa kuingiza timu tano kutoka hatua ya makundi na kucheza hatua ya 16 bora msimu huu.

Celtic v Zenit, Arsenal watacheza dhidi ya Ostersunds katika hatua ya timu 32 bora ya Ligi ya Ulaya au Uefa ndogo kama inavyojulikana na wengi.

Chelsea ndio timu eee ya Uingereza kufuzu hatua ya 16 bora kama mshindi wa pili swa kundi lake, huku timu zingine nne zikiongoza katika makundi yao.

The Blues (Chelsea) ndio inaonekana kuwa na kibarua kigumu zaidi kwa timu za Uingereza katika hatua hiyo ya 16 bora na kuiweka katika wakati mgumu wa kuvuka hatua hiyo kutokana na ukali pamoja na uzoefu wa Barcelona inayoongozwa na Lione Messi.

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya kocha wa Chelsea Antonio Conte kusema kuwa nafasi ya timu yake kutetea taji la Ligi Kuu imetoweka baada ya timu hiyo kupokea kivhapo cha kutoka kwa West Ham, ambacho kimewaacha wakiwa nyuma hya Manchester City kwa pointi 14.

Hatahivyo, Chelsea iliifunga Barcelona katika nusu fainali kabla ya kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa wa Ulaya mwaka 2012.

Real Madrid, ambayo iko mbioni kutwaa taji la 13 na la tatu mfululizo, nayo imepewa timu ngumu ya PSG, ambayo imetumia fedha kwa ajili ya usajili  na imemaliza nyuma ya Tottenham katika Kundi H.

Washindi wa makundi watakuwa ugenini katika mchezo wa kwanza wa hatua hiyo ya 16 bora Februari 13 au 14 na Februari 20/21, na nyumbani katika mchezo wa marufdiano utakaofanyika kati ya Machi 6/7 na Machi 13/14.

Fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya itafanyika Mei 26 Kiev,

RATIBA KAMILI YA HATUA YA 16 BORA YA LIGI YA MABINGWA WA ULAYA:-

Juventus v Tottenham (Februari 13 na Machi 7, 2018)

Basel v Manchester City (Februaria 13 na Machi 7, 2018)

Porto v Liverpool (Februari 14 na Machi 6, 2018)

Sevilla v Manchester United (Februari 21 na Machi 13, 2018)

Real Madrid v PSG (Februari 14 na Februaria 6, 2018)

Shakhtar Donetsk v Roma (Februari 21 na Machi 13, 2018)

Chelsea v Barcelona (Februari 20 na Machi 14, 2018)


Bayern Munich v Besiktas (Februari 20 na Machi 14, 2018)

No comments:

Post a Comment