Friday 29 December 2017

Familia ya Kizimbabwe Yakaa Airport kwa miezi mitatu

BANGKOK, Thailand
KAWAIDA hakuna mtu ambaye hufurahia kukaa muda mrefu katika kiwanja cha ndege, lakini imekuwa tofauti kwa familia moja ya Wazimbabwe, ambao Kiwanja cha Ndege cha Bangkok kumekuwa nyumbani kwao kwa karibu miezi mitatu sasa.

Kwa mujibu wa Idara ya Uhamiaji ya Thailand, watoto wanne wenye umri chini ya miaka 11 na watu wazima wanne waliwasili mjini hapa tangu Mei, lakini waligoma kurejea kwao Zimbabwe wakihofia kufunguliwa mashtaka.

Watu hao walibainika baada ya mtu mmoja ambaye alisema kuwa alikuwa akifanya kazi katika Kiwanja cha Ndege cha Suvarnabhumi alipotupia picha katika mtandao wa Facebook ikimuonesha akitoa zawadi ya Krismads kwa msichana mdogo wa kiafrika.

Kwa sasa picha bhiyo ikiwaimeondolewa, Kanaruj Artt Pornsopit alisema familia hiyo imekuwa ikiishi kiwanjani hapo kwa karibu miezi mitatau sasa “kwa sababu ya hali isiyo ya usalama” nchi humo.

"Natumaini wote mtarejea nyumbani kwenu haraka iwezekanazo,”alisema.
Msemaji wa Idara ya Uhamiaji Pol Col Cherngron Rimphadee alisema familia hiyo awali iliwasili Thailand kama watalii. Walijaribu kupanda ndege kuondoka Bangkok Oktoba kwenda jiji la Hispania la Barcelona kupitia Kiev huko Ukraine.

Lakini walizuiwa kupanda ndege kwa sababu hawakuwa na viza inayowaruhusu kuingia Hispania.

Hatahivyo, pia walizuiwa kuingia Thailand baada ya awali kukaa muda zaidi kuliko viza yao ya awali ilivyokuwa ikiwaruhusu kwa miezi mitano hivyo ilibidi kulipa faini.


Baadae familia bhiyo ilifanya utaratibu mwingine na ndege ya Kimataifa ya Ukraine (UIA) badala yake walipitia Kiev kwenda Dubai na baadae walipita nchi ya tatu kutaka kuingia Ulaya kama wahamiaji.

No comments:

Post a Comment