Wednesday 13 December 2017

Moody Sheli ndiye Mr Tanzania Fitness 2017

Moody Sheli (mbele) akiwaongoza wenzake katika moja ya mazoezi kwenye viwanja vya Leaders Club Kinondoni jana.
Na Mwandishi Wetu
MOODY Sheli ametwaa ubingwa wa Mr Tanzania Fitness baada ya kuwashinda washiriki wengine 29 katika mpambano uliofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.

Katika shindano hilo washiriki walichuana katika michuano mbalimbali ikiwa kubeba vyma, kupiga pushapu, kukimbia na mazoezi mengine mbalimbali, ambapo Sheli alinekana kungara zaidi.

Nafasi ya pili ilichukuliwa na watu wawili, ambao walifungana kwa pointi ambao ni Eric Majura pamoja na Obadia Andabwile huku nafasi ya tatu ikienda kwa Martine Njessa.


Mwenyekiti wa Shirikisho la Mchezo wa Kujenga Mwili Tanzania, TBBF, Nemes Chiwalala akitete jambo wakati wa shindano la kumsaka Mr Tanzania Fitness kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.
Kilele cha shindano la kumsaka Mr Tanzania 2017 kitafanyika kesho Ijumaa katika ukumbi wa hoteli ya May Fair Plaza Mikocheni Jijini Dar es Salaam, ambapo mshindi atapatikana, ambapo washindi wataondoka na zawadi nono likiwemo gari aina ya Noah na sh milioni 10 kwa mshindi wa kwanza.

Leo Alhamisi litafanyika shindano la kumsaka mshiriki maarufu zaidi katika mitandao ya kijamii.










No comments:

Post a Comment