Friday 7 October 2016

Ukata waisumbua timu ya taifa ya Nigeria `Super Eagles'



ABUJA, Nigeria
TIMU ya taifa ya Nigeria itachelewa kufika katika mchezo wa kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2018 dhidi ya Zambia baada ya kuahirisha kuondoka kutokana na matatizo ya fedha.

Timu hiyo sasa itabidi kuwasili saa 22 tu kabla ya mchezo wake huo uliopangwa kupigwa Jumapili nchini Zambia katika mbio za kusaka kufuzu kwa fainali zitakazofanyika Urusi.

Wachezaji wa timu hiyo badala ya kuondoka mapema sasa walitarajia kuondoka leo kwenda Zambia.

Kwa ratiba hiyo kikosi cha timu hiyo sasa kinatarajia kutua leo mchana, na kinatarajia kufanya mazoezi mara moja tu kabla ya kuikabili Zambia kesho Jumapili.

Amaju Pinnick, kiongozi wa Shirikisho la Soka la Nigeria (NFF), aliiambia kamati ya michezo ya Bunge kuwa NFF inakabiliwa na ukata wa kulipia ndege ya kukodi na malazi.

Kiongozi wa NFF pia alithibitishi kuwa wachezaji wanaocheza soka Ulaya wametakiwa kujilipia tiketi zao za ndege na kutumia daraja la kawaida ili kujiunga na kambi ya timu hiyo katika mji mkuu wa Nigeriua, Abuja.

Mwezi uliopita, timu ya taifa ya Olimpiki ya Nigeria iliwasili saa chache kabla ya mechi yao ya kwanza kutokana na matatizo ya usafiri.

No comments:

Post a Comment