Sunday 30 October 2016

Kidosho wa Kinondoni awa Miss Tanzania 2016 aondoka na gari na fedha taslimu


Miss Tanzania 2016 Diana Edward akipunga mkono akiwa pamoja na washindi wa pili na tatu, Grace Malikita (kushoto) na Mary Peter mara baada ya shindano hilo lililofanyika Rock City Mall  jijini Mwanza juzi. (Na Mpigapicha Wetu).

Na Mwandishi Wetu
ALIYEKUWA Miss Kinondoni Dayana Edward ndiye mlimbwende wa Tanzania 2016 baada ya kuwashinda wenzake 29 katika viwanja vya Rock City Mall juzi usiku mkoani hapa. 

Mashindano hayo makubwa kabisa hapa nchini yaliamuliwa na majaji ambao ni Rita Mbelo,Catherine Kibaso,Sophia Masei,Raphael Siantini,Joe Makanyaga,Eliza Kilili,Juma Sultan,Prashant Patel na Ramesh Shah.

Mashindano hayo yalianza kwa warembo kucheza nyimbo mbali mbali kabla ya kutinga na mavazi ya ubunifu,ufukweni na vazi la jioni.

Jaji Shah aliweza kuwataja warembo walioingia 15 bora ambao ni Anna Nitwa,Sia Pius,Lisa Ndolo,Grace Malikita,Eunice Robert,Regina Ndimbo,Iluminata Dominic,Sporah Lulende na Maria Peter. 

Wengine ni Maureen Ayoub,Queen Nazir,Julietha Kabete,Maureen Kamanya na Abel John. 

Patel aliwataja warembo walioingia 5 bora ambao ni Grace Malikita,Anna Nitwa,Maria Peter,Julietha Kabete na Dayana Edward. 

Jaji Prashant Patel aliweza kutangaza warembo walioingia tatu bora, ambao ni Dayana Edward aliyeibuka mshidi, huku nafasi ya pili ikachukuliwa na Grace Malikita wakati Maria Peter alimaliza watatu.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,Annastazia Wambura aliomba mshindi wa shindano hilo ajitahidi kuzingatia nidhamu na uzalendo haswa pale atakapo wakilisha nchini katika mashindano ya mrembo wa dunia. 

Wambura alisistiza waandaji wa mashindano hayo waendelee kufuata taratibu za mashindano na kuhakikisha wanatekeleza mikataba waliosaini na warembo hao. 

Wambura ameomba mashindano hayo yafanyike katika mikoa mengine pia tofauti na hapa.

Dayana alikabidhiwa gari aina ya Toyota IST yenye thamani ya sh milioni 14.

No comments:

Post a Comment