Monday 10 October 2016

Costa, Nolito watupia Hispania ikiibuka na ushindi dhidi ya Albania katika mbio za kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018




Timu ya taifa ya Iceland, ikipunga kwa mashabiki baada ya mchezo wa kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2018 dhidi ya Uturuki jana huko Reykjavik, Iceland. Iceland ilishinda mabao 2-0.

MADRID, Hispania
MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Diego Costa na Nolito wa Manchester City walizifumania nyavu wakati Hispania ikiifunga Albania na kuongoza katika Kundi G katika mechi za mbio za kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018 kwa Kanda ya Ulaya.

Wachezaji wa Ligi Kuu ya England David de Gea, Nacho Monreal na David Silva wote waliichezea Hispania katika mchezo huo walioibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Katika kundi hilo hilo, Italia ilihitaji takribani dakika 91 ili kupata bao la ushindi lililofungwa na Ciro Immobile na kutoka nyuma na kuichapa Macedonia.

Mshambuliaji wa Lazio Immobile alisawazisha mapema kwa Italia wakati ilipocheza na timu inayoshikilia nafasi ya 146 katika viwango vya ubora wa soka duniani.

Kwingineko katika Kundi G, Israel iliifunga Liechtenstein 2-1 kwa bao la mshambuliaji wa Brighton Tomer Hemed alipofunga mabao yote mawili kwa wenyeji.

Mshambuliaji wa Newcastle United Aleksandar Mitrovic alifunga mara mbili, kabla ya kiungo wa Southampton Dusan Tadic hajapachika bao la ushindi, wakati Serbia ikiichapa Austria kwa mabao 3-2.

Kwa matokeo hayo, Serbia inaoongoza Kundi D ikiwa juu ya Jamhuri ya Ireland na Wales.

Croatia inaoongoza katika Kundi I baada ya mshambuliaji wa Juventus Mario Mandzukic kuipatia timu hiyo ushindi wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Finland.

Iceland ni ya pili kufuatia ushindi wa mabao 2-0 ilioupata dhidi ya Uturuki na katika kundi hilo hilo, Ukraine iliichapa Kosovo 3-0.

No comments:

Post a Comment