Thursday 20 October 2016

TOC yatangaza taratibu za kuchukua na kurejesha fomu kwa wanaotaka kugombea uongozi




Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) akizungumza na waandishi wa habari leo katika ofisi zilizopo Mwananyamala jijini Dar es Salaam kuhusu Uchaguzi Mkuu wa kamati hiyo utakaofanyika Desemba 10 Dodoma. Kulia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji Irine Mwasanga.
Na Mwandishi Wetu
Ndugu Waandishi wa Vyombo vya Habari mbalimbali za Michezo,

Habari za Asubuhi!!!

Kwa mara nyingine tumekutana tena ili tuweze kuwapa baadhi ya taarifa za shughuli ambazo Kamati ya Olimpiki Tanzania huzifanya na kuzitekeleza kwa mujibu wa Katiba yetu ya TOC.

Leo katika muhadhara huu  kwa niaba ya Kamati ya Olimpiki Tanzania napenda kuchukua nafasi hii kuwaarifu mambo matatu (3) muhimu ambayo mara kwa mara Waandishi mbalimbali wa Habari hasa za Michezo wamekuwa wakiyauliza:

1. Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Kamati ya Olimpiki
    Tanzania.

2. Utambaulisho wa Kamisheni ya Kusimamia Uchaguzi wa
    TOC.

3. Taarifa ya Uchaguzi wa Kamisheni ya Wachezaji.

Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi. Kushoto ni Mhazini Mkuu wa TOC, Charles Nyange na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TOC, Irine Mwasanga.
a. Taarifa ya Uchaguzi wa TOC:
         Uchaguzi huu ambao utafanyika mwaka huu kwa
         mujibu wa Katiba ya TOC (Ibara ya 20 Para 1)
         utafanyika Dodoma  Disemba 10, 2016.

 Ufuatao ni utaratibu mzima wa Maandalizi ya Uchaguzi wa
 TOC:-
a.  Uchukuaji wa Fomu za Wagombea zitaanza
     kutolewa katika   ofisi za TOC (Tanzania Bara na
     Zanzibar) tarehe  25/10/2016 na kurejeshwa tarehe

Mwenyekiti wa Kamati ya wanawake ya Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Irine Mwasanga akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi.
     15/11/2016 (Katiba ya TOC Ibara ya 23 para  2.)
         b.  Ada ya Fomu ya Wagombea  zitauzwa na ofisi ya
              TOC (Bara na Zanzibar) kwa gharama zifuatazo:
               i.  200,000.00 (Rais, Makamu wa Rais, Katibu
      Mkuu, Katibu Mkuu Msaidizi, Mhazini Mkuu, na
      Mhazini Mkuu Msaidizi)
              ii. 150,000.00 (Wajumbe)
         c.  Kurejesha Fomu:
              Fomu zitarejeshwa Ofisi Kuu na Ndogo za TOC
              zilizoko Mwananyamala, Jengo la Shirika la Nyumba
              la Taifa (Biashara Complex) ghorofa ya tatu na
              Uwanja wa Amani, Zanzibar tarehe 15/11/2016 kabla
              ya saa 10.00 mchana. Fomu hazitapokelewa baada
              ya tarehe na muda huo.

         d.  Kuhakiki Fomu baada ya kurejeshwa:
              18/11/2016: Kamisheni itakutana Dar Es Salaam
               ili kupitia na kuzihakiki fomu zote tayari kwa usaili.

         e.  Usaili wa Wagombea:
              Usaili wa Wagombea utafanyika:
              i.   22/11/2016 (Dar Es Salaam, Tanzania)
              ii.  24/11/2016 (Zanzibar, Tanzania)
                   Usaili utafanyika kwa lugha ya Kiswahili na
                   Kiingereza.

         f.  Kutangaza Matokeo:
             Tarehe 30/11/2016: Kamisheni ya Uchaguzi itakutana
             na Waandishi wa Vyombo vya Habari katika ofisi ya
             TOC Dar Es Salaam kutangaza majina  ya Wagombea
              waliopitishwa.

         g. Malalamiko:
             Baada ya kutangazwa matokeo, kama kutakuwa na
             malalamiko, yatapokelewa na kusikilizwa kuanzia
             siku baada ya majina ya wagombea
             yatakapotangazwa (30/11/2016).


         h. MUHIMU: 
 i.  Sifa ya Mgombea:
     Kama ilivyooanishwa katika  Katiba ya TOC (Ibara
     ya 22 para 1-10).
               ii.  Ikiwa mgombea jina lake halikupitishwa na
                    atahitaji  maelezo ya sababu za jina lake
                    kutopitishwa, Kamisheni ya Uchaguzi ina wajibu
                    wa  kumfahamisha na kumridhisha mgombea
                    sababu za jina lake kutopitishwa.

Kila mgombea  atakayepitishwa ambaye siyo Mjumbe wa Kamati ya Utendaji inayomaliza muda wake atapaswa kujilipia gharama zake zote za kwenda na kujikimu atakapokuwa Dodoma wakati wa uchaguzi (10/12/2016).
1.  Utambulisho wa Kamisheni ya Kusimamia Uchaguzi wa
     TOC.
     Katika kikao chake cha tatu (3) kilichofanyika  Zanzibar
     hapo tarehe 27/08/2016, Kamati ya Utendaji ya TOC 
     ilipendekeza Kamisheni itakayosimamia Utaratibu mzima
     wa uchaguzi wa viongozi wa TOC kwa miaka 4 ijayo.
     (Katiba ya TOC, Ibara ya 21, Kipengele Na. 6)
       Kamisheni  hiyo ya watu watatu (3) ilikuwa na Wajumbe
       wafuatao:-
a. Lloyd Nchunga-Tanzania Bara
b. Harrison Chaulo-Tanzania Bara
c. Abdallah Juma Mohamed-Zanzibar

Kamisheni hiyo hapo juu itasimamia Maandalizi na Uchaguzi Mkuu wa TOC tu.

TAARIFA YA UCHAGUZI WA KAMISHENI YA WACHEZAJI TANZANIA (KAWATA)
Uchaguzi huu utafanyika  mjini Dodoma tarehe 8/12/2016 siku mbili kabla ya Uchaguzi Mkuu wa TOC.

Kamisheni ya Wachezaji Tanzania (KAWATA) ilifanya uchaguzi wake mjin Dodoma tarehe 06/12/2012.

Ni matuimaini ya Kamati ya Olimpiki Tanzania kwamba,  KAWATA Taifa imefanya kazi kubwa ya kuvihamasisha Vyama/Mashirikisho ya Michezo kufanya chaguzi zao tangu kwa kufuata mwongozo wao.

KAWATA Taifa iko chini ya Ulezi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania, kama ilivyo Kamisheni ndani ya Vyama/Mashirikisho ya Michezo kuwa chini ya ulezi wao Vyama/Mashirikisho  hayo.

Kwa muongozo wa KAWATA, Kamisheni ya Taifa na Vyama/Mashirikisho ya Michezo inatakiwa kuwa na Wajumbe wasiopungua 5 na kuzidi 8.
Nafasi zitakagombewa:
1. Mwenyekiti
2. Katibu
3. Wajumbe 4/6 (Kwa idadi sawa ya jinsia)

Fomu za Wagombea zitatolewa na kurejeshwa tarehe 28/10/2016 na 11/11/2016 kabla ya saa 10.00 mchana katika ofisi za TOC Tanzania Bara na Zanzibar.

Wagombea ambao hawatakuwa Wajumbe wa Kamisheni ya Chama/Shirikisho la Mchezo husika watakaohudhuria Mkutano Mkuu mjini Dodoma tarehe 8/12/2016 itawalazimu kujilipia gharama ya kwenda Dodoma mara tu majina yaliyopitishwa yatakapotangazwa.

Maandalizi na Usimamizi wa Uchaguzi wa KAWATA  utafanywa na Sekretariat ya Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC).

No comments:

Post a Comment