Monday 10 October 2016

Mzambia kutua Yanga na benchi jipya kabisa la ufundi kumbadili Hans van der Pluijm


George-Chicken-Lwandamina; Anayetarajia kuchukoa mikoba ya Mholanzi Hans van der Pluijm.

Na Mwandishi Wetu
YANGA inatarajia kubadilika mara utakapomalizika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara Novemba 6 mwaka huu baada ya uongozi kutaka kubadili benchi lote la ufundi la timu hiyo, imedokezwa.

Kimsimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga iko katika nafasi ya sita baada ya kujikusanyia pointi 11 kufuatia kushuka dimbani mara sita nafasi ambayo haijaufurahisha uongozi wa klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani.

Taarifa kutoka ndani ya Yanga zinasema kuwa benchi lote la timu hiyo litaondoka na kuja sura mpya ikiongozwa na kocha Mzambia, George Lwandamina atakayesaidiwa na Charles Mkwassa, Manyika Peter kama kocha wa makipa na meneja Sekilojo Chambua.

Kocha Mkuu Hans van der Pluijm raia wa Uholanzi na wasaidizi wake, Juma Mwambusi, kocha wa makipa Juma Pondamali na Meneja Hafidh Saleh wote wazalendo wataondoka.
 Mazungumzo yanaendelea, tutakapokubaliana atakuja kusaini,kilisema chanzo hicho cha ndani.

Na kuhusu watendaji wapya wa benchi la Ufundi wazalendo, chanzo kimesema; Hao wote wamependekezwa na kwa kuwa ni watu wetu, ni suala la kuzungumza nao tu,.

Pluijm amejikuta katika wakati mgumu baada ya Yanga kuambulia pointi 11 kati ya 18 za mechi sita za Ligi Kuu Tanzania Bara.

Yanga SC imetoa sare mbili, imefungwa mechi moja na kushinda tatu tangu kuanza kwa Ligi Kuu hiyo ikiwa ni mbali na kupoteza mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC kwa penalti 4-1 baada ya sare ya 2-2.

Na baada ya mchezo wa Oktoba 1, wakalazimishwa sare ya 1-1 na mahasimu wao, Simba waliokuwa pungufu kwa sehemu kubwa kufuatia kutolewa kwa kadi nyekundu kwa nahodha wao, Jonas Mkude katika dakika ya 29, baadhi ya viongozi wa Yanga wamependekeza mwalimu huyo aondolewe
 

No comments:

Post a Comment