Friday 3 August 2018

Wakazi wa Simiyu Wapata Maelezo ya Ujenzi wa Kiwanja Kipya cha Ndege cha Mkoa Wao Kutoka Kwenye Banda la Maonesho ya 88 la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania

Bi. Elizabeth Manoti mkazi wa Simiyu akisikiliza kwa makini maelezo mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa leo na Ofisa Tehama Mwandamizi, Bw. Geofrey Youze katika banda la maonesho ya Kilimo na sherehe za Nanenane la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), yanayofanyika kwenye Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Mhandisi Alexander Kalumbete (mwenye kofia)  wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), akiwaeleza wakazi wa Mkoa wa Simiyu kwa kuwaonesha picha za Kiwanja kipya cha ndege kinachotarajiwa kujengwa eneo la Igegu mkoani hapa, leo walipotembelea banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane yanayoendelea kwenye Viwanja vya Nyakabindi.

Wanafunzi kutoka shule ya Sekondari ya Ngulyati ya Bariadi mkoani Simiyu wakipata maelezo ya viwanja vya ndege kutoka kwa Mwanasheria Mwandamizi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bi. Janet Mugini leo.

Ofisa Biashara na Masoko Mwandamizi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bi. Herieth Nyalusi, akiwaeleza wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Ngulyati ya Bariadi leo walipotembelea banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane la TAA, yanayofanyika kwenye Uwanja wa Nyakabindi.
Mtangazaji Fred Mwanjala wa Kituo cha televisheni cha Channel 10 akimhoji  Ofisa Mipango na Takwimu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Edward Kimaro leo alipotembelea banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane yanayofanyika kwenye uwanja wa Nyakabindi.
Wananchi mbalimbali wakipata maelezo ndani ya banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), yanayoendelea kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu  leo. 
Ofisa Usalama Mwandamizi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Bakari Mwalwisi akielezea Bw. Geronimo Gelle wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) juu ya ubebaji wa vimiminika kwenye mizigo inayowekwa kwenye begi la mkononi.       

No comments:

Post a Comment