Friday 3 August 2018

Sita Wauawa Vurugu za Uchaguzi nchini Zimbabwe

Mtu akipita katika moja ya mitaa mjini Zimbabwe pembeni ya duka lililovunjwa vioo na waandamanaji.

HARARE, Zimbabwe
MJI Mkuu wa Zimbabwe, Harare uligeuka mji wa vurugu, chini ya saa 24 baada ya watu sita kuuawa katika mapambano ya wapinzani na watu wa usalama kupinga matokeo ya uchaguzi uliofanyika Jumatatu.

Askari walitumia jana asubuhi kuondoa shughuli zote na kuwaonya watu kuondoka haraka hadi ifikapo mchana siku hiyo. Magari iliweka misururu mirefu, ambayo kila mmoja alikuwa akijaribu kupita.
Vijana wakileta vurugu baada ya Uchaguzi Mkuu wa Zimbabwe.

Maduka yalifungwa, huku polisi wa kuzuia ghasia waliizungua makao makuu ya chama cha upinzani cha Movement for Democratic Change na kuzuia mitaani yote ua jirani.

Polisi iliwakamata watu 18 wakati walipoiweka chini ya ulinzi Makao Makuu ya MDC, ambapo msemaji wa Jeshi la Polisi la Zimbabwe, Charity Charamba alisema, bado mashtaka hayajawa tayari, lakini Charamba alisema tayari watu 26 wametiwa mbaroni wakituhumiwa kuleta virugu wakati wa maandamano juzi.
Askari akitokea kisago kwa raia mmoja aliyedaiwa kuleta vurugu.

Wakati wakitangaza idadi mpya ya watu waliokufa, ibidi wanajeshi kuingia mitaani baada ya hali kutokuwa nzuri na hivyo kuhitajika nguvu zaidi kutumika ili kuleta amani.


No comments:

Post a Comment