Thursday 30 August 2018

Nditiye aiagiza TAA kufanya ukaguzi wa mwisho wa viwanja vya wananchi waliohamishwa Kipawa ili wakabidhiwe

NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) , Richard Mayongela leo kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa eneo la kuondokea na kuwasili abiria mashuhuri, VIP. 

Na Mwandishi Wetu
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, ameagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, wakakague viwanja 537 vilivyotengwa maeneo ya Msongola, kwa ajili ya waliokuwa wakazi wa eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam Jumanne wiki ijayo ili kujiridhisha kama viwanja hivyo vipo na  vinafaa.

Mhandisi Nditiye ametoa agizo hilo leo Agostri 30, 2018, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwe nye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam ambapo alieleza wasiwasi wake kuwa kampuni iliyopewa kandarasi ya kuwatafutia viwanja wananchi hao haijatekeleza wajibu wake ipasavyo licha ya kuwa tayari imelipwa kiasi cha shilingi bilioni 3.7.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, TAA, Richard Mayongela akimkaribisha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (kushoto) ili azungumze na waandishi wa habari baada ya kutembelea TAA.

“Nakuagiza Mkurugenzi wa TAA, kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Wilaya Jumanne ijayo muende mkakague eno hilo la viwanja 537 muone kama vipo kwa sababu kumekuwa na shida sana na hawa wenzetu wa Tanzania Remix Centre  nyinyi wenyewe mnajua, kuna shida ya miundombinu, sasa lazime mjue eneo hilo linafikika, na viwanja hivyo vinajengeka.” Alisema

Ofisa Tarafa wa Ukonga Jijini Dar es Salaam, Nicodemus Shirima akizungumza wakati wa ziara hiyo ya Naibu Waziri Nditiye. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Paul Rwegasha.
Alisema Wananchi wako tayari kushirikiana na serikali katika kuhakikisha upanuzi wa uwanja unakwenda vizuri.

Kampuni ya Tanzania Remix Centre ilipendekezwa na Manispaa ya  Ilala na kupewa kandarasi ya kutafuta viwanja kwa ajili ya makazi mapya ya wananchi waliokuwa wakiishi eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo kulikuwepo na mivutano kati ya Mamlaka na Wananchi ambapo baadhi yao walipeleka shauri hilo mahakamani na hiovyo kufanya zoezi hilo la kuwahamisha wananchi hao kwenye eneo hilo jipya kusuasua.
Rosemary Shimata, mwakilishi kutoka Tanzania Remix Centre.

Hata hivyo akitoa taarifa kwa Mhe. Naibu Waziri Nditiye, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw.Richard Mayongela alisema, Novemba mwaka jana, TAA ilikutana na wadau wakiwemo wananchi, Manispaa ya Ilala, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Kampuni iliyoingia ubia na Manispaa ya Ilala katika kutafuta viwanja kwa ajili ya wananchi hao.

“Mradi huu ulihusisha upatikanaji wa viwanja 1,600 kwa mujibu wa mkataba wa awali ambapo fidia yake ilipaswa kufanywa kwa awamu mbili ya watu 800, hata hivyo kwa mujibu wa sheria kipinde kile ilitaka mwananchi apewe eneo lakini alipwe fidia pia.” Alisema na kufafanua kuwa.

NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye akizungumza na waandishi wa habari alipofanya ziara Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, TAA. Mwingine ni Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Richard Mayongela.
“Sasa wananchi wa Kipawa na Kigilagila walilipwa fidia kwa mujibu wa sheria na kwao hakukuwa na tatizo, kwa maana walipewa fedha taslimu na viwanja maeneo ya Pugu Mwakanga.” Alisema Bw. Mayongela

Akieleza zaidi Bw. Mayongela alsiema Baada ya kufanya tathmini, ilibainika kuwa wananchi wa Kipunguni A na Kipunguni Mashariki ambapo kulikuwa na viwanja 1,186 baada ya kufanya tathmini viwanja vilivyohitajika siyo 1,600, bali ni 1,186, kwa ajili ya fidia ya wananchi wa maeneo hayo mawili na katika viwanja hivyo viwanja 537 serikali ilishatoa kiasi cha shilingi bilioni 3.7 ili kutekeleza zoezi hilo.
 
Sisi kwa kushirikiana na mbia wa Mnaispaa ya Ilala yaani Tanzania Remix Centre, tukaandaa vile viwanja na viwanja vile vimeshapatikana na kuanzia hivi sasa, viwanja hivyo vitagawiwa kwa wananchi.

Aidha, katika hatua nyingine, Mhe. Nditiye amesema wakati umefika sasa kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, kuanzisha kitengo cha Estate ili kihakikisha viwanja vyake vyote nchini vinakuwa na hati miliki.

NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (kushoto) akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, TAA, Richard Mayongela baada ya Nditiye kuzungumza na waandishi wa habari.
“Naguagiza uunde kitengo cha Estate kisichozidi watu 10 ili kihakikishe kila kiwanja kinachomilikiwa na TAA kinakuwa na hati miliki na hii itaepusha migogoro na wananchi.” Alisema.

No comments:

Post a Comment