Thursday 30 August 2018

UEFA Yapanga Makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya, Nyota Cristiano Ronaldo Kukutana na Man United


ZURICH, Uswisi
MANCHESTER United itaungana na Cristiano Ronaldo baada ya kupangwa na mabingwa wa Ligi Kuu ya Italia, Serie A, Juventus katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Ronaldo, ambaye aliichezea Man United kwa mafanikio makubwa katika miaka ya 2003 na 2009, alijiunga na Juve kwa gharama ya pauni milioni 99.2 mwezi uliopita baada ya miaka tisa ya kuitumikia Real Madrid.

Valencia na Young Boys ni timu zingine zilizopangwa katika Kundi H.
Tottenham wenyewe wamepnagwa katika kundi gumu, ambapo itawabidi kukabiliana na wakali Barcelona, wakati washindi wa pili wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu huu, Liverpool watakabiliana na Paris St-Germain (PSG) na Napoli.

Mabingwa PSV Eindhoven na Inter Milan wanakamilisha Kundi B, ambalo pia litakuwa na timu ya England Tottenham  na Red Star Belgrade ni timu nyigine ambayo itacheza na kikosi cha kocha Jurgen Klopp katika Kundi C.

Mabingwa wa Ligi ya England Manchester City wamepangwa katika Kundi F pamoja na Shakhtar Donetsk, Lyon na Hoffenheim.

Mabingwa watetezi Real Madrid, ambao wameshinda taji hilo kwa miaka mitatu mfululizo, wenyewe wako katika Kundi G pamoja na Roma, CSKA Moscow na Viktoria Plzen.

Ratiba Kamili ya Makundi:
Kundi A: Atletico Madrid, Borussia Dortmund, Monaco na Club Brugge.

Kundi B: Barcelona, Tottenham, PSV Eindhoven na Inter Milan.

Kundi C: Paris St-Germain, Napoli, Liverpool na Red Star Belgrade.

Kundi D: Lokomotiv Moscow, Porto, Schalke na Galatasaray.

Kundi E: Bayern Munich, Benfica, Ajax na AEK Athens.

Kundi F: Manchester City, Shakhtar Donetsk, Lyon na Hoffenheim.

Kundi G: Real Madrid, Roma, CSKA Moscow na Viktoria Plzen.

Kundi H: Juventus, Manchester United, Valencia na Young Boys.

No comments:

Post a Comment