Thursday 2 August 2018

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) watoa huduma kwenye maonesho ya Kilimo 88 mkoani Simiyu


Ramadhani Mawazo (kushoto) akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa maafisa wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kutoka kulia Geofrey Youze, Mhandisi Alexander Kalumbete na Bakari Mwalwisi kwenye maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika katika Uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu. 
      Ofisa Usalama Mwandamizi wa Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bakari Mwalwisi (kushoto) akitoa maelezo yanayohusiana na ulinzi na usalama kwenye viwanja vya ndege kwa wakazi wa Simiyu waliotembelea banda la maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika kwenye Uwanja wa Nyakabindi.


   Mwanasheria Mwandamizi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bi. Janeth Mugini (kulia) akimfafanulia mambo mbalimbali Bi. Grace Mgombera mkazi wa Simiyu alipotembelea banda la maonesho ya Kilimo Nanenane la TAA.
 Kikosi kazi cha maonesho ya Kilimo kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wakiwa kwenye picha ya pamoja katika banda lao maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika kwenye uwanja wa Nyakabindi.
Bw. Masaga Malika (kulia) akimsikiliza Mhandisi Alexander Kalumbete akimpa maelezo ya ujenzi wa Kiwanja kipya cha Ndege cha mkoa wa Simiyu, katika banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) katika maonesho ya Kilimo Nanenane.


Mhandisi Alexander Kalumbele (kulia) akitoa maelezo mbalimbali yanayohusu Viwanja vya Ndege Tanzania kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA), Bi. Vumilia Zikankub (wa pili kulia) aliyeongozana na Bw. Mikalu Mapunda, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara (kushoto) na Bw. Chambua Majuto (wa pili kushoto).   
 Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA), Bw. Mohamed Ally (mwenye miwani kushoto), alipotembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwenye viwanja vya maonesho ya Kilimo Nanenane, yanayofanyika Nyakabindi mkoani Simiyu.


No comments:

Post a Comment