Tuesday 21 August 2018

Simba Yafungua Pazia Ligi Kuu na Tanzania Prisons kesho


Na Mwandishi Wetu
MABINGWA wa Ligi Kuu Bara, Simba ksho wanaingia kwenye mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa Ligi hiyo kuwakabili Tanzania Prison katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Simba inashuka dimbani kama Bingwa mtetezi baada ya kutwaa kombe hilo msimu uliopita ikiwa na pointi 69 nyuma ya Azam waliokuwa na 58.

Simba inaingia uwanjani ikiwa na hali ya kujiamini baadaa ya jumamosi iliyopita kutwaa ubingwa wa Ngao ya jamii na hasa uwepo wa kikosi kipana chenye wachezaji wenye uwezo mkubwa.

Ni wazi kuwa Simba itapambana katika kuhakikisha inapata pointi tatu kwani ilifanya jitihada za kutosha katika kujindaa na msimu wa Ligi hiyo baada ya kuweka kambi ya wiki mbili nchini Uturuki.

Kocha wa timu hiyo Patric Aussems alisema kikosi chake kimefanya maandalizi ya kutosha kuelekea mchezo huo na kudai kuwa michezo ya kirafiki ilikuwa ni kwa lengo la kuangalia sehemu zenye matatizo.

“Nimetumia michezo ya kirafiki kama maandalizi ya Ligi Kuu nina imani na kikosi kilichopo,ila kuna wachezaji walipata tatizo na kutolewa dhidi ya Mtibwa hivyo nitasikiliza ripoti na wengine watatumika,”alisema Aussems.

Kocha huyo anaimani kuwa kikosi chake kitafanya vizuri kwani pamoja na kukerwa na mbinu ya wachezaji wake kutumia mipira mirefu aliahidi kulifanyia kazi suala hilo.

Michezo mingine ya Ligi hiyo itakuwa ni Ruvu Shooting na Ndanda, Alliance na Mbao Fc,Coast Union na Lipuli ya Iringa, Singida na Biashara Mara na mchezo mwingine ni Kagera Sugar na Mwadui ya Shinyanga.


No comments:

Post a Comment