Sunday 5 August 2018

RC Simiyu Afurahishwa na Maelezo ya Banda la TAA

      Mshauri wa Sera za Miundombinu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Bi. Pudencia akimsikiliza kwa makini Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela jana wakati akielezewa masuala mbalimbali alipotembelea banda la mamlaka hiyo katika Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane yanayofanyika kwenye Uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Jumanne Sagini (wa pili kushoto) akipata taarifa ya ujenzi wa Kiwanja kipya cha Ndege cha mkoa huo kutoka kwa Mhandisi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Alex Kalumbete jana alipotembelea banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane yanayofanyika kwenye Uwanja wa Nyakabindi. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kushoto) jana akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (watatu kushoto) alipotembelea banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane la Mamlaka yanayofanyika kwenye uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (aliyenyoosha mkono) jana akimwonyesha chati yenye viwanja 58 vya ndege Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka alipotembelea banda la maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane la Mamlaka yanayofanyika kwenye uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Kamati ya maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), jana alipotembelea banda la Mamlaka hilo katika Uwanja wa Nyakabindi. Kulia waliokaa ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw. Richard Mayongela.

No comments:

Post a Comment