Tuesday 7 August 2018

Manchester United Yagoma Kumuachia Pogba


MANCHESTER, England
KLABU ya Manchester United imetupilia mbali ofa ya Barcelona ya kiasi cha pauni milioni 45  ya kutaka kumnunua Paul Pogba pamoja na kuwatoa Yerry Mina na Andre Gomes, kwa mujibu wa Sky nchini Italia.MANCHESTER, England

KLABU ya Manchester United imetupilia mbali ofa ya Barcelona ya kiasi cha pauni milioni 45  ya kutaka kumnunua Paul Pogba pamoja na kuwatoa Yerry Mina na Andre Gomes, kwa mujibu wa Sky nchini Italia.

Taarifa hizo zinafuatia ripoti ya awali kutoka kwa wakala wa Pogba, Mino Raiola, ambaye alisafiri hadi mjini hapa katika jaribio la kutaka kumchukua mchezaji huyo wa Man United ili kwenda kwa mabingwa hao wa Hispania kwa ajili kiungo huyo Mfaransa.

Lakini United kwa sasa haina mpango wa kuachana na Pogba, ambaye ndio kwanza amerejea katika mazoezi baada na kushinda taji la Kombe la Dunia akiwa na Ufaransa.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, alisajiliwa na Man United mwaka 2016 – kwa ada iliyokuwa rekodi ya dunia kwa wakati huo ya pauni milioni 93.25, na amebakisha miaka mitatu katika mkataba wake wa sasa.

Hata kama United itataka kumuuza mchezaji huyo, kesho Alhamisi ndio siku ya mwisho ya dirisha la usajili la Ligi Kuu ya England, ambapo wana siku mbili tu kumpata mchezaji atakayechukua nafasi yake.

Dirisha la usajili halitafungwa Hispania hadi Agosti 31, hiyo ikiwa na maana kuwa Barcelona wana nafasi hadi mwishoni mwa mwezi kujaribu kumsajili Pogba (pichani) katika kipindi hiki cha usajili.


Taarifa hizo zinafuatia ripoti ya awali kutoka kwa wakala wa Pogba, Mino Raiola, ambaye alisafiri hadi mjini hapa katika jaribio la kutaka kumchukua mchezaji huyo wa Man United ili kwenda kwa mabingwa hao wa Hispania kwa ajili kiungo huyo Mfaransa.

Lakini United kwa sasa haina mpango wa kuachana na Pogba, ambaye ndio kwanza amerejea katika mazoezi baada na kushinda taji la Kombe la Dunia akiwa na Ufaransa.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, alisajiliwa na Man United mwaka 2016 – kwa ada iliyokuwa rekodi ya dunia kwa wakati huo ya pauni milioni 93.25, na amebakisha miaka mitatu katika mkataba wake wa sasa.

Hata kama United itataka kumuuza mchezaji huyo, kesho Alhamisi ndio siku ya mwisho ya dirisha la usajili la Ligi Kuu ya England, ambapo wana siku mbili tu kumpata mchezaji atakayechukua nafasi yake.

Dirisha la usajili halitafungwa Hispania hadi Agosti 31, hiyo ikiwa na maana kuwa Barcelona wana nafasi hadi mwishoni mwa mwezi kujaribu kumsajili Pogba katika kipindi hiki cha usajili.

No comments:

Post a Comment