Tuesday 31 October 2017

Tottenham, Real Madrid kuwania kutinga mchujo

LONDON, England

TOTTENHAM na Real Madrid zinakutana kesho katika moja ya mechi za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, huku kila moja ikiwa na nafasi ya kufuzu kucheza kwa hatua ya 16 bora kutoka katika Kundi H.

 

Timu yoyote itakayoshinda kesho inaweza kufuzu kucheza hatua hiyo, ambayo inajulikana kama raundi ya mwanzo ya mtoano.

 

Tottenham Hotspur FC na mabingwa watetezi Real Madrid zinakutana kwenye Uwanja wa Wembley, kila moja ikijua umuhimu wa mchezo huo katika kusonga mbele katika mashindano hayo.

Baada ya timu hizo kutoka sare ya kufungana 1-1 katika mchezo wao wa kwanza uliofanyika kwenye Uwanja wa Santiago Bernabéu Hispania katika raudi ya tatu, timu hizo zinalingana kwa pointi kileleni mwa msimamo wa kundi lao.

Timu hizo zinalingana kila kitu katika msimamo wa kundi hilo, ambapo kila moja ina pointi saba, huku Tottenham ikiongoza na kufuatiwa na Real.

 

Timu zinazofuata katika msimamo wa kundi hilo, Borussia Dortmund na APOEL FC kila moja ina pointi moja.

Tottenham haijawahi kuifunga Madrid, ambapo imepoteza mechi tatu kati ya tano walizokutana huko nyuma, huku wakitoka sare mara mbili.

 

Bao la kujifunga la Raphaël Varane katika mchezo wao watatu ndio pekee, ambao Tottenham imewahi kufunga ilipocheza dhidi ya Real Madrid katika dakika 450 walizocheza.

MECHI WALIZOKUTANA

Mchezo wa kwanza wa Tottenham kukutana na Real Madrid katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya ulikuwa katika msimu wa mwaka 2010/11, ambao ulimalizika kwa Real kushinda 4-0 nyumbani katika mchezo wa kwanza wa robo fainali.

Mabao hayo yalifungwa na Emmanuel Adebayor katika dakika ya nne na 57 na mengine yaliwekwa kimiani na Ángel Di María (72) na Cristiano Ronaldo (87), huku Tottenham ikicheza muda mwingi wakiwa 10 baada ya Peter Crouch kutolewa nje baada ya kupewa kadi ya pili ya njano katika dakika ya 15.

 

Ronaldo ndiye aliyefunga bao pekee katika mchezo wa marudiano uliofanyika kwenye Uwanja wa White Hart Lane wakati Merengues wakikamilisha ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Tottenham, ambayo ilikuwa na akina Gareth Bale na Luka Modrić, ambao wote kwa sasa wapo Real Madrid.

MAN CITY VS NAPOLI

Mchezo mwingine wa leo utakaovuta hisia za wapenzi wengi wa soka ni ule utakaowakutanisha vinara wa Ligi Kuu ya England, Manchester City dhidi ya Napoli.

Manchester City haijafungwa hata mchezo mmoja na imejikusanyia pointi tisa baada ya kushuka dimbani mara tatu, inacheza na Napoli iliyopo katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi tatu tu.

Man City inataka kushinda mchezo huo wa leo ili kuzidi kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kutoka katika Kundi F.

MECHI ZINGINE

Mechi zingine kesho zitakuwa kati ya Beşiktaş            itakayocheza dhidi ya Monaco wakati Sevilla            itaikaribisha Spartak Moskva huku Shakhtar Donetsk ikipepetana na Feyenoord.


Mechi nyingine ni Liverpool itakuwa na kibaruia kizito kwenye uwanja wake wa Anfield wakati itakapoikaribisha Maribor huku Porto   itacheza dhidi ya RB Leipzig,na Borussia Dortmund            watacheza na APOEL.

Makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya

Kundi F

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Manchester City33008179
2Shakhtar Donetsk32014406
3Napoli31025503
4Feyenoord300329-70

Kundi G

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Beşiktaş33007259
2RB Leipzig311145-14
3Porto31026603
4Monaco301226-41

Kundi H

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Tottenham Hotspur32107257
2Real Madrid32107257
3Borussia Dortmund301237-41
4APOEL301217-61

No comments:

Post a Comment