Monday 23 October 2017

Neymar atolewa wakati PSG ikitoka sare

Neymar  akioneshwa kadi nyekundu wakati PSG ilipocheza dhidi ya Olympique de Marseille.

PARIS, Ufaransa

NEYMAR alitolewa nje kabla ya mchezaji mwenzake Edinson Cavani akithibitisha thamani yake kwa mara nyigine tena kwa kufunga bao la kusawazisha katika dakika za mwisho wakati Paris St Germain (PSG) ikitoka sare ya 2-2 dhidi ya wapinzani wao wakubwa Olympique de Marseille.

Mshambuliaji huyo wa Uruguay alisawazisha dakika moja ndani ya muda wa nyongeza kwa shuti kali la umbali wa kama meta 20 baada ya Neymar kutolewa nje katika dakika ya 87 kwa kadi ya pili ya njano.

Neymar ndiye alikuwa wa kwanza kuipatia timu yake bao la kusawazisha katika dakika ya 33 kufuatia lile la kuongoza la Olympique de Marseille lililofungwa na Luiz Gustavo katika dakika ya 16.

Awali, Marseille walifunga bao la pili katika dakika ya 78 lililowekwa kimiani na Thauvin, ambalo baadae PSG walisawazisha kupitia kwa Cavan na kunusurika kupata kipigo cha kwanza.

Kimsimamo, PSG ina pointi 26 baada ya kucheza mechi 10 ikiwa kileleni pointi nne zaidi ya Monaco iliyopo katika nafasi ya pili.

 

"Ni bao muhimu kwani mchezo ni kama ulikuwa umemalizika, lakini angalau tumeondoka na pointi, “alisema Cavani.


Monaco wako nafasi ya pili, pointi nne nyuma wakiwa na pointi 22 baadaya kuifunga Caen 2-0 Jumamosi.

No comments:

Post a Comment