Tuesday 24 October 2017

Chaneta walivyokabidhiana `ofisi' Uwanja wa Taifa

Mwenyekiti mpya wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta), Devota Marwa akizungumza baada ya kukabidhiwa nyaraka mbalimbali za chama hicho na mwenyekiti wazamani Annie Kibira kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wazamani wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta) akizungumza kabla ya kukabidho `ofisi' kwa mwenyekiti mpya wa chama hicho, Dk Devota Marwa. Kulia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji Kilongozi Mohamed. Makabidhiano hayo yalifanyikia kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Makamu mwenyekiti wazamani wa Chaneta, Zainabu Mbiro akipanda katika gari la Chama jhicho aina ya Noah wakati akilikabidhi kwa uongozi mpya wa Chaneta kwenye Uwanja wa Taifa. 

Mwenyekiti Mpya wa Chaneta, Dk Devota Marwa akikagua garia aina ya Noah baada ya kukabidhia nyaraka mbalimbali na uongozi uliopita pamoja na gari hilo.
Mwenyekiti wazamani wa Chaneta, Annie Kibira (kushoto) akimkabidhi Katiba mwenyekiti mpya wa chama hicho, Dk Devota Marwa wakati wa makabidhiano ya `ofisi' yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia katikati ni Ofisa Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa, Bahati Msofe.

No comments:

Post a Comment