Friday 27 October 2017

Fifa yaongeza zawadi Kombe la Dunia

ZURICH, Uswisi

MATAIFA 32 yatakayoshindana katika fainali za Kombe la Dunia 2018 yatagawana kiasi cha dola za Marekani milioni 400 (sawa na sh bilioni 898) katika zawadi ikiwa ni ongezeko la asiliia 12 ya fedha za mashindano ya mwaka 2014, Fifa imesema.

Katika taarifa yake jana Shirikisho hilo la Kimataifa la Soka limesema kuwa fedha zawadi katika mashindano yaliyopita yaliyofanyika Brazil zilikuwa dola za Marekani milioni 358.

Imeelezwa kuwa Ujerumani ambaye ni bingwa wa Kombe la Dunia alindoka na kitita cha dola za Marekani milioni 35, huku mshindi wa pili Argentina alipata dola milioni 25.

Tofauti, nchi ambazo zitashindwa kuvuka hatua ya makundi kila moja itapokea kiasi cha dola za Marekani milioni 8.

Katika mkutano wa Fifa uliofanyika Kolkata, bodi hiyo ya Fifa pia imepitisha taratribu za kuomba uenyeji wa Kombe la Dunia kwa ajili ya mwaka 2026.

Huku ikithibitisha tarehe za mashindano mbalimbali, yakiwemo ya Kombe la Dunia yatakayofanyika Falme za Kiarabu na yale ya wanawake ya mwaka 2019 yatakayofanyika Ufaransa.


Fainali za Kombela Dunia za mwaka 2018 zitafanyika kuanzia Desemba 12 hadi 22, wakati yale ya wanawake ya mwaka 2019 yamepangwa kufanyika kuanzia Juni 7 huku fainali ikifanyika Julai 7.

No comments:

Post a Comment