Monday 23 October 2017

SuperSport uso kwa uso na TP Mazembe Shirikisho

Kikosi cha mabingwa wa Kombe la Shirikisho la Afrika,TP Mazembe

JOHANNESBURG, Afrika Kusini

TIMU ya SuperSport United ilikuwa imekamilika karibu katika kila idara wakati ikifuzu kwa fainali ya Kombe la Shirikisho 2017 baada ya kushinda mabao 3-1 dhidi ya Club African.

Kwa ushindi huo, SuperSport ya Afrika Kusini imetinga fainali kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya mchezo huo wa nusu fainali ya pili uliofanyika kwenye Uwanja wa Stade Olympique Radès Jumapili.

Mchezo wa kwanza wa nusu fainali ulifanyikia kwenye Uwanja wa Lucas Moripe, ambao ulimalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1.

Kwa matokeo hayo, SuperSport itakutana na bingwa mtetezi TP Mazembe, ambayo iliifunga FUS Rabat ya Morocco, katika fainali ya mechi mbili za nyumbani na ugenini mwezi ujao.


Wachezaji wa SuperSports United.

Bradley Grobler aliwafungia wageni, huku Jeremy Brockie naye pia alizifumania nyavu wakati Saber Khalifa aliwafungia wenyeji bao la kufutia machozi.

No comments:

Post a Comment