Tuesday 24 October 2017

Ronaldo, Zidane wang'ara tuzo za Fifa 2017

LONDON, England

CRISTIANO Ronaldo ametangazwa kuwa ndiye mchezaji bora wa dunia wa kiume katika tuzo za Shirikisho la Kimataifa la Soka 2017 zilizofanyika jijini hapa.

Mshambuliaji huyo wa Real Madrid na Ureno aliwapiga kumbo mwenzake wa Barcelona Lionel Messi na yule wa Paris St-Germain, Neymar katika mbio za kutwaa tuzo hiyo.

Ronaldo, 32, aliisaidia Real Madrid kutwaa mataji mawili, likiwa lile le La Liga, ambalo walilitetea na La Liga msimu wa mwaka 2016-17.

Lieke Martens wa Barcelona na Uholanzi alishinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia wakike, huku kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane alitangazwa kuwa kocha bora wakiume na Mholanzi Sarina Wiegman amekuwa kocha bora wakike.

Mchezaji wa Arsenal Olivier Giroud alipokea tuzo ya Puskas kwa ajili ya bao lake bora 2017 walipocheza dhidi ya Crystal Palace Januari.

Tofauti ya Ballon d'Or na Fifa?

 

Hii ni mara ya pili kufanyika tuzo hizo za Fifa za soka, ambazo ni tofauti na zile za Ballon d'Or.

Tuzo ya Ballon d'Or ilikuwa ikitolewa na jarida la Soka la Ufaransa tangu mwaka 1956, lakini Fifa ilijitenga na tuzo hizo na kuanzisha zake.

Badala yake, ilianzisha tuzo za tuzo za mchezaji bora wa Fifa, ambapo Ronaldo ndiye alikuwa mchezaji wa kwanza kutwaa tuzo hiyo Januari.

Kura za kumpata mchezaji na kocha bora zinapigwa na manahodha wa timu za taifa na makocha, waandishi wa habari walioteuliwa, na kwa mara ya kwanza, kura za katika mtandao zilipigwa na mashabiki. Kila kundi lilikuwa na asilimia 25 ya kura.

Cristiano Ronaldo

Ni mwaka mwingine wa kuvutia kwa Ronaldo, ambaye aliyetwaa tuzo ya kwanza ya mchezaji bora wa Fifa wa Dunia baada ya kuiongoza Ureno kutwaa taji la Euro 2016.

Mwaka huu alifunga mabao mawili wakati Real Madrid ikishinda 4-1 dhidi ya Juventus katika fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na pia alizifumania nyavu mara 25 katika mechi 29 alizoichezea klabu yake katika La Liga ikiwa ni kwa mara ya kwanza katika miaka mitano.

 

"Tuko England kwa mara ya kwanza, na tumeshinda kwa mara ya pili mfululizo. Huu ni wakati mzuri kwangu, “alisema Ronaldo alipokuwa akizungumza wakati wa kukabidhiwa tuzo hiyo.

Wachezaji watatu wakiume

Cristiano Ronaldo - 43.16 %  Lionel Messi - 19.25 %           Neymar - 6.97%

Messi alimpigia kura mchezaji mwenzake wa Barcelona Luis Suarez kama mchezaji bora, wakati Ronaldo naye pia alimpigia mchezaji mwenzake wa Real, Luka Modric.

Kocha wa England Gareth Southgate alimpigia kura Ronaldo.

 

Mchezaji bora wakike

Martens, 24, alikuwa mhimili wa timu ya taifa ya Uholanzi katika ushindi wa timu hiyo katika mashindano ya Mataifa ya Ulaya, ambapo alishinda tuzo ya mashindano hayo.

Fifpro World XI

 

Fifa imefanya mabadiliko matatu katika kikosi cha mwaka 2016. Kipa Gianluigi Buffon alimbadili Manuel Neuer, wakati mchezaji wa AC Milan Leonardo Bonucci alimbadili mchezaji wa Barcelona, Gerard Pique katika nafasi ya beki bora na mchezaji wa PSG Neymar ameshika nafasi ya ushambuliaji bora hiyo badala ya Luis Suarez.

Orodha ya wachezaji hao watano ni kutoka Real Madrid, wawili Barcelona, wawili PSG, mmoja Juventus na mmoja AC Milan. Hakuna mchezaji wa Ligi Kuu ya England aliyomo katika kikosi hicho.

Kocha bora

Real ilimaliza msimu uliopita ikiwa bingwa wa Hispanuia na kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2012 na kutwaa ubigwa wa Ulaya kwa mara ya pili mfululizo.

Zidane alishinda tuzo hiyo akimshinda kcha wa Chelsea Antonio Conte, ambaye alitwaa taji la Ligi Kuu katika msimu wake wa kwanza England, na yule wa Juventus, Massimiliano Allegri, aliyeiongoza timu yake kutwaa mataji mawili ya Serie A na lile la Coppa Italia.

 Makocha watatu wakiume

Zinedine Zidane - 46.22%      Antonio Conte - 11.62%           Massimiliano Allegri - 8.78%

Kocha bora wakike

Mholanzi Wiegman alioongoza timu yao ya taifa kutwaa taji la Euro 2017 katika ardhi ya nyumbani, ambapo timu hiyo ilicheza soka safi la kuvutia.

Hilo lilikuwa taji lao la kwanza kubwa la kimataifa kwa timu ya wanawake baada yakuifunga Denmark katika fainali.

Tuzo ya Puskas

Bao bora la mwaka 2017 ni lile lililofungwa na mchezaji wa Arsenal, Giroud.

Bao hilo lilifungwa katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Palace siku ya mwaka mpya, ambapo mshambuliaji huyo Mfaransa alifunga bao safi aliunganisha krosi ya Alexis Sanchez niliyopigwa nyuma yake.

Kipa bora

Bingwa wa Kombela Dunia, na mshindi mara 10 wa taji la Serie A, Gianluigi Buffon ndiye mshindi wa kwanza wa tuzo ya kipa bora.

Kipa huyo mkongwe aliisaidia Juventus kutwaa mara sita mfululizo taji la Serie A na kucheza dakika 600 bila kuruhus bao katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.


Buffon, 39, alitwaa tuzo hiyo akiwashinda Keylor Navas, Manuel Neuer, aliyeisaidia Bayern Munich kutwaa Bundesliga.

No comments:

Post a Comment