Sunday 21 May 2017

Nyota ya Samatta yaendelea kung'ara Ubelgiji

Na Mwandishi Wetu
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta usiku wa jana amecheza vizuri kwa dakika zote 90 timu yake, KRC Genk ikilazimisha sare ya 1-1 ugenini dhidi ya Lokeren Uwanja wa Daknam mjini Lokeren, Ubelgiji kwenye mchezo wa Kundi B kuwania tiketi ya kucheza michuano ya Ligu ndogo ya UEFA mwakani.

KRC Genk walitangulia kwa bao la penalti la kiungo mkongwe wa umri wa miaka 33, Mbelgiji Koen Persoons aliyejifunga dakika ya nne, kabla ya mshambuliaji mwenye umri wa miaka 31, Mbelgiji pia Tom De Sutter kuisawazishia Lokeren dakika ya 57.


Pamoja na sare hiyo, Genk inaendelea kuongoza Kundi B katika mchuano wa kuwania tiketi ya Europa League mwakani kwa kufikisha pointi 26 baada ya kucheza mechi tisa na Samatta jana ameichezea Genk mechi ya 58 tangu ajiunge nayo Januari mwaka jana kutoka TP Mazembe ya DRC akiwa amefunga mabao 19.

No comments:

Post a Comment