Sunday 21 May 2017

Arsenal yashindwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya

Mshambuliaji wa Everton, Kevin Mirallas (kulia) akikimbizwa na mchezaji wa Arsenal Alex Iwobi (katikati) wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England leo kwenye Uwanja wa Emirates Jijini London. Arsenal ilishinda mabao 3-1.
LONDON, England
PAMOJA na kushinda mabao 3-1 dhidi ya Everton katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya England, Arsenal imeshindwa kufuzu kucheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kumaliza  katika nafasi ya tano.

Timu hiyo ambayo ilianza siku ikiwa pointi moja nyuma ya Liverpool iliyokuwa katika nafasi ya nne, ilionekana kama ingeweza kumaliza ya nne baada ya kupata bao la kuongoza katika dakika ya nane.
Lakini Liverpool, ilihitaji ushindi tu wa aina yoyote ili imalize katika nafasi ya nne, ambapo ilianza kuifunga Middlesbrough kabla ya mapumziko na kuibuka na ushndi wa mabao 3-0.

Manchester City yenyewe ilimaliza ya tatu baada ya kupata ushindi rahisi wa mabao 5-0 dhidi ya Watford.

Ligi ya Ulaya kwa Arsenal

Hatua ya Arsenal kufuzu kucheza Ligi ya Ulaya kwa mara ya 19 mfululizo ilifikia tamati jana baada ya kumaliza katika nafasi ya tano.

Imani ilikuwepo kwa mashabiki wa nyumbani wakati Hector Bellerin alipoifungia the Gunners bao la mapema huku taarifa zikizagaa kuwa, Liverpool ilikuwa katika wakati mgumu dhidi ya wapinzani wao Hull City ambao tayari walishashuka daraja.
Kiungo wa Liverpool, Georginio Wijnaldum (kushoto) akiwania mpira pamoja na mchezaji wa Middlesbrough, Grant Leadbitter walati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Anfield mjini Liverpool, kaskazini magharibi ya England.
Liverpool sasa itacheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kwa mara ya kwanza tangu ilipofanya hivyo kwa mara ya mwisho msimu wa mwaka 2014-15.

Manchester City ilitwaa nafasi ya tatu na kufuzu moja kwa moja kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kushinda 5-0 dhidi ya Watford.

Mabingwa Chelsea imekuwa timu ya kwanza ya Uingereza kushinda mara 30 katika ligi kubwa katika mechi 38 za msimu mmoja wakati timu hiyo ikimuaga nahodha wao wa muda mrefu, John Terry huku ikipata ushindi mnono wa 5-1 dhidi ya Sunderland.

The Blues, ambayo imetwaa ushindi wake wa sita wa Ligi Kuu siku tisa zilizopita, ilijikuta nyuma baada ya bao la mapema la Javier Manquillo lakini ilijibu mapema kupitia Willian.

Eden Hazard alifunga bao lake la 17 la msimu na kuifanya timu yake kuongoza kabla nafasi yake haijachukuliwa na Pedro.

Katika mechi zingine za ligi hiyo, Burnley ilifungwa na West Ham mabao 2-1 huku Hull City ikipokea kichapo cha mabao 7-1 kutoka kwa washindi wa pili wa ligi hiyo, Tottenham.


No comments:

Post a Comment