Thursday 11 May 2017

Eritrea yatamba kushinda riadha ya vijana Dar

Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya riadha ya Eritrea kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 wakiwa mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam tayari kwa mashindano hayo yatakayoanza kesho Jumamosi kwenye uwanja huo.
Na Mwandishi Wetu
TIMU ya taifa ya Eritrea imesema kuwa itafanya vizuri katika mashindano ya riadha ya Kanda ya Tano ya Afrika yatakayoanza Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kiongozi wa msafara wa timu hiyo, ambaye pia ndiye rais wa Shirikisho la Riadha la Eritrea, Bereket Mesfun alisema jana jijini kuwa, timu yao imejiandaa vizuri na imekuja kushinda.

Alisema hali ya hewa ya sasa ya Dar es Salaam wameifurahia sana na inafana na ile ya kwano, hivyo itawasidia kufanya vizuri pia.
Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT), Wilhelm Gidabuday (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu mashindano ya riadha ya Kanda ya Tano ya Afrika yatakayofanyika Jumamosi. Kulia ni mjumbe  wa Kamati ya Utendaji ya RT, Tullo Chambo.
Naye Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT), Wilhelm Gidabuday alisema kuwa jumla ya nchi saba zitashiriki katika mashindano hayo badala ya 11 za awali.

Gidabuday alizitaja nchi zilizothibitisha kuwa ni pamoja na Eritrea, ambayo tayari imetua nchini na Sudan Kusini ilitarajia kuwasili jana kwa njia ya barabara.
Nyingine ni Kenya, Sudan, Zanzibar, Somalia pamoja na wenyeji Tanzania Bara, ambayo timu yao leo itahamishia kambi jijini Dar es Salaam kutoka Kibaha tayari kwa mashindano hayo.


No comments:

Post a Comment