Tuesday 29 December 2015

Sare na Chelsea yampa kiburi Van Gaal na kusema kamwe hatojiuzulu ng'oo



Kocha Mkuu wa Man United, Louis van Gaal (kushotot) akiangalia timu yake ikitoka suluhu na Chelsea pamoja na msaidizi wake, yan Giggs.

LONDON, England
KOCHA wa Manchester United, Louis van Gaal anasema kuwa kamwe hatajiuzulu licha ya kushuhudia timu yake ikiteleza hadi nje ya nne bora katika msimamo wa Ligi Kuu ya England.

Suluhu ya Jumatatu nyumbani dhidi ya helsea ina maana kuwa, Man United sasa imeshindwa kuibuka na ushindi katika mechi nane katika mashindano yote.

Hiyo haijawahi kuwatokea tangu mwaka 1990 na kuiacha klabu hiyo ikiwa pointi tano nyuma ya wapinzani wao wa jiji Manchester City ambao wako katika nafasi ya nne katika msimamo huo.

Lakini bado Van Gaal alikuwa na moyo na kusema: "Wakati wachezaji wanaonesha kiwango kama kile pamoja na shinikiza kibao, kwa kweli hakuna sababu ya kuachia ngazi.

'Wachezaji wako Tayari Kupambana'
Siku chache zilizopita kocha, ambaye alianza kuifundisha Man United tangu Julai mwaka jana, alikuwa majaribuni.

Mholanzi huyo mwenye umri wa miaka 64 aliibuka kabla ya Krismas baada ya vyomo vua habari kukosoa nafasi yake.

Baadae timu yake ilipokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Stoke, kipigo kilichoongeza shinikizo la kutimuliwa huku ikidaiwa kuwa nafasi yake inaweza kuchukuliwa na Jose Mourinho, aliyetimuliwa na Chelsea Desemba 17.

Kabla ya mchezo huo wa Jumatatu dhidi ya the Blues, baadhi ya mashabiki walikuwa wamebeba skafu zenye jina la Mourinho, ambazo zilikuwa zinauzwa nje ya Uwanja wa Old Trafford.

No comments:

Post a Comment