Wednesday 9 December 2015

Mourinho: Kila timu inataka kucheza na Chelsea katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya



LONDON, England
KOCHA WA Chelsea Jose Mourinho anaamini kuwa wapinzani wao katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kila moja anataka apanwe na timu yake katika hatua ya 16 bora.

The Blues wamemaliza washindi wa Kungi G baada ya jana usiku kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Porto, ikiwa na maana kuwa wanatarajiwa kupangwa dhidi ya moja ya timu sita zilizomaliza katika nafasi ya pili katika makundi yao
Ratiba hiyo ya hatua ya 16 itapanwa Jumatatu.

Chelsea inaweza kupanwa ama na Paris St-Germain, Juventus, PSV Eindhoven, Benfica, Roma au Gent.

"Kila timu iliyomaliza katika nafasi ya pili inataka kucheza na sisi (Chelsea) au Zenit St Petersburg," alisema Mourinho mwenye umri wa miaka 52.

Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England wamekuwa na wakati mgumu katika ligi hiyo ya nyumbani ambapo wamepoteza mechi nane kati ya 15 walizocheza katika ligi hiyo msimu huu na kujikuta wakiwa katika nafasi ya 14.

Lakini timu hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika mashindano ya Ulaya ambapo imeshinda mechi nne na kutoka sare moja katika mechi zao sita za hatua ya makundi na kutina hatua ya mtoano ya michuano hiyo.

The Blues walikata tiketi ya kucheza hatua hiyo ya 16 bora kupitia kwa Ivan Marcano aliyejifunga katika kipindi cha kwanza huku bao safi la Willian akilifunga baada ya mapumziko.

"Kila timu inaogopa kucheza na Barcelona, hawataki kucheza na Real Madrid, hawataki kucheza na Atletico, hawapendi kusikia wanapanwa kucheza na Bayern Munich," aliongeza Mourinho.

Mourinho ana nia ya kuwa kocha wa kwanza kutwaa mara tatu taji la Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na klabu tatu tofauti, ambapo aliziongoza Porto na Inter Milan kutwaa taji hilo mwaka 2004 na 2010.

Na kocha huyo Mreno anasema Blues, licha ya kufanya ibaya katika ligi ya nyumbani, inaweza kuwazishangaza zile timu zinazopewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa.

"Timu ambayo inachechemea ni wazi sio mshindani katika mbio a ubingwa kwa sababu kuna timu bora zaidi Ulaya alisema ourinho, ambaye aliwahi pia kuiongoza Real Madrid kati ya mwaka 2010 na 2013.

"Lakini hata tulipotwaa taji na Porto hatukuwa washindani. Na hata tulishinda na Inter Milan hatukuwa washindani wa taji hilo.

"Wakati tulipokuwa washindani tuliwa na Real Madrid tulishindwa katika robo fainali, na tulipoteza nusu fainali mbili na Chelsea.

Muhimu: Timu nane zilizoshikamnafasi ya kwanza katika makundi yao zinapanwa na nane zilizoshika nafasi ya pili, inawa timu kutoka nchi moja kamwe haziwezi kupanwa pamoja katika hatua hiyo ya 16 bora,

Pia timu zilizowahi kukutana katika hatua ya makundi haziwezi kupanwa pamoja katika hatua hiyo inayofuata.

Kutokana na utaratibu huo inamaana kuwa Chelsea haiwezi kucheza dhidi ya Arsenal au Dynamo Kiev katika hatua hiyo ya 16 bora.

TIMU ZILIZOFUZU KWA 16 BORA:

Real Madrid, Paris St-Germain, Wolfsburg, PSV Eindhoven,
Atletico Madrid, Benfica,Manchester City, Juventus,Barcelona,
Roma, Bayern Munich, Arsenal, Chelsea, Dynamo Kiev, Zenit St Petersburg na Gent.

No comments:

Post a Comment