Tuesday 1 May 2018

Liverpool Yapata Pigo Ikicheza na Roma Ulaya


LONDON, England
JURGEN Klopp amepata pigo kubwa kuelekea mchezo wao wa marudiano wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya dhidi ya Roma baada ya msaidizi wake muhimu Zeljko Buvac kuachia ngazi kutokana na sababu za kibinafsi.

Huku Liverpool ikiwa mbioni kukabiliana na Roma katika mji mkuu wa Italia Jumatano usiku, klabu hiyo imethibitisha juzi kuwa Buvas atakuwa nje ya timu hiyo hadi mwishoni mwa msimu.

Klopp alimuelezea Buvas kama "kichwa" katika suala zima la ukocha na kutokuwepo kwake ni pigo kubwa kwa Liverpool ambayo inaangalia kuendelea ushindi wake wa awali wa mabao 5-2 dhidi ys Roma.

Tetesi zilianza kusambaa tangu Jumapili kuwa Bosnian anaachia ngazi, lakini Liverpool ilikanusha taarifa hizo kwa kusisitiza kuwa Buvac bado ni muajiriwa wa klabu hiyo na pengo lake halitaathiri kitu.

Buvac, ambaye alikuwa katika benchi pamoja na Klopp katika mchezo wa Jumamosi ambao timu hiyo ilitoka suluhu dhidi ya Stoke, alikuwa msaidizi wa karibu kabisa wa kocha huyo Mjerumani katika kipindi cha miaka 17 iliyopita.

Wawili hao walikuwa pamoja huko Mainz katika miaka ya 1990 na waliungana tena wakati Klopp alipomfanya kuwa msaidizi wake wakati alipokuwa kocha mwaka 2001.

Wakati alivyopanda pamoja wawili hao walienda Borussia Dortmund mwaka 2008 ambako walishinda mfululizio taji la Bundesliga na kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kabla hawajahamia Liverpool.

Wakati huohuo, leo inashuka nchini Italia kucheza dhidi ya Roma katika mchezo wa pili wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Kikosi cha Klopp kiko mbioni kutinga fainali baada ya kuwa na faida ya mabao mengi iliyopata katika mchezo wa kwanza ilipoifunga Roma mabao 5-2, ikiwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 2007 walipofikia hatua ya juu ya mashindano makubwa Ulaya.

Lakini nje ya uwanja presha ni kubwa wakati shabiki wa Liverpool Sean Cox lyuko katika koma baada ya kushambuliwa kabla ya mchezo wa wili iliyopita uliofanyika kwenye Uwanja wa  Anfield.

Mashabiki wawili wa Roma walikamatwa kuhusiana na jaribio hilo la kutaka kuuwa na gwiji wa klabu hiyo Francesco Totti ametaka kuwepo kwa mchezo wa kiungwana, na kuheshimiwa kwa wapinzani.

Mshambuliaji wazamani wa Roma Mohamed Salah alifunga mara mbili na kutengeneza mengine mawili wakati Liverpoo; ikizifumania nyavu mara tano kwenye Uwanja wa Anfield kabla ya mawili yaliyofungwa katika dakika za mwisho.

Kikosi cha Klopp kitashuka uwanjani bila ya kiungo Alex Oxlade-Chamberlain, ambaye atakuwa nje ya uwanja kwa msimu mzima kutokana na maumivu ya goti, pamoja na Georginio Wijnaldum ambaye alibadilishwa katika mchezo wa kwanza.

Emre Can (mgongo) na Adam Lallana (maumivu ya nyama za paja) nayo pia wanapambana na maumivu.

No comments:

Post a Comment