Monday 14 May 2018

Conte Akata Tamaa ya Ubingwa FA Cup


LONDON, England
KOCHA Antonio Conte anadai Chelsea haina nafasi ya kushinda fainali ya Kombe la FA dhidi ya Manchester United isipokuwa kama itajiimarisha haraka baada ya kuhoji uwezo wa wachezaji wake.

Kocha huyo Mhitalia alisema kikosi hicho kinatakiwa kuboreshwa baada ya kupokea kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Newcastle United Jumapili na kumaliza msimu vibaya na kushindwa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Kikosi cha Conte kilikuwa na nafasi ya kumaliza ligi juu ya nafasi ya tano, lakini sasa watacheza Ligi ya Ulaya, wana nafasi ya kutwaa taji wakati watakapocheza dhidi ya Man United kwenye Uwanja wa Wembley Mei 19.

Hilo linatarajia kuwa pambano la mwisho kwa Conte katika kikosi hicho cha Chelsea, ambacho kitacheza dhidi ya kocha wao wazamani Jose Mourinho, kocha huyo mwenye umri wa miaka 48  anajua kuwa klikosi chake kinahitaji kuinua kiwango chake katika idara zote ili kutwaa taji kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2012.

"Tulitaka kumaliza msimu katika njia nzuri, lakini tungeweza kufanya vizuri zaidi ya hivi, “alisema.

"Kwa hilo, nimekuwa wa kwanza kujibu kuhusu mchezo mbovu. Newcastle walionesha mchezo mzuri na kupambana, na kama tutacheza kama hivi katika fainali ya Kombe la FA, basi kamwe hatutakuwa na nafasi.

"Tuna siku sita tu kubadili muelekeo wetu, na tunatakiwa kupambana kwasababu tunaweza kufanya vizuri zaidi.”

Amebakisha miezi 12 kabla ya kumalizika kwa mkataba wake wa sasa, na alipoulizwa kuhusu hatma yake, kocha huyo wazamani wa timu ya taifa ya Italia aliongeza: “Nina mkataba, na najituma na klabu inajua kila kitu.

"Mchezo wa Jumamosi ndio utakuwa wa mwisho? Hapana, sifikiri hivyo. Kitu muhimu ni klabu, na sio uvumi kuhusu mimi.”

No comments:

Post a Comment