Saturday 19 May 2018

Mwanafunzi Auwa 10 kwa Risasi Marekani


TEXAS, Marekani
WATU 10 wameuawa huku wengine 10 wakijeruhiwa baada ya mwanafunzi mmoja kuvurumisha risasi katika shule ya sekondari ya Texas, gavana wa jimbo hilo amesema.;

Mshambuliaji huyo, ambaye alikamatwa na kushitakiwa kwa mauaji, alifahamika kwa jina la Dimitrios Pagourtzis, ni mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 katika Shule ya Santa Fe High School.

Alidaiwa kutumia binduki aina ya mashine gani ambayo aliichukua kutoka kwa baba yake, ambaye alikuwa akimiliki bundiki hiyo kihalali.
 
Wengi waliokufa katika tukio hilo ni wanafunzi, polisi ilisema katika tukio hilo.

Gavana wa Texas, Greg Abbott alisema "vimekuta katika shule hiyo aina tofauti tofauti ya vilipuzi, maili 40 (kilometa 65 kusini mwa Hoston.

Abbott alisema polisi ilikuta taarifa katika shajala ya mtuhumiwa huyo , komputa na simu ya mkononi akidai kuwa alipanga kufanya shambulizi hilo na baadae kujiua.

Gavana huyo alisema kuwa kijana huyo “alijisalimisha kwa sababu halikosa ujasili wa kujiua.”
 
Mkuu wa Polisi wa Santa Fe, Jeff Powell aliwataka wakazi wa eneo hilo kuwa makini na vitu vyovyote watakavyoviona nakuwataka kutoa taarifa polisi haraka. “Mshishike kitu chochote mtakachokiona.”

Ofisa polisi wa shule ya Santa Fe John Barnes ametajwa kuwa mmoja wa walioumia. Yuko katika hali mbaya na amefanyiwa upasuaji, kilieleza chombo kmoja cha habari mjini hapa.

No comments:

Post a Comment