Monday 14 May 2018

Salah Aweka Rekodi ya Mabao Ligi Kuu England


LONDON, England
MOHAMED Salah ameweka rekodi mpya ya kufunga mabao katika Ligi Kuu baada ya kupachika mabao 32 katika mechi 38 alizocheza na kuuhakikishia Liverpool nafasi ya kurejea katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu ujao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Brighton katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Anfield.

Ushindi huo kwa Liverpool unamaana kuwa haijalishi Chelsea imepata matokeo gani katika mchezo wake dhidi ya Newcastle United, lakini ilifungwa mabao 3-0 katika mchezo wake uliofanyika kwenye Uwanja wa St James's Park.

Chelsea hata kama ingeshinda bado isingeweza kumaliza katika nafasi ya nne, kwani Liverpool ilitakiwa kufungwa ndio Chelsea ifuzu kwa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu ujao.
 
Liverpool imepania kutwaa taji la sita Ulaya wakati itakapokutana na Real Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya Mei 26.

Lakini vijana wa Jurgen Klopp wanajua kuwa hata kama hawata twaa taji katika fainali hiyo huko Kiev, watarejea katika Ligi ya Mabingwa msimu ujao baada ya kuisambaratisha Brighton ugenini katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya England.

"Sasa tuko katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu ujao na nimepata tuzo pia, hivyo ninajivunia sana, “alisema Salah wakati akikabidhia tuzo ya kiatu cha dhahabu kwa ufungaji bora katika Ligi Kuu ya England.

Mabingwa wapya Manchester City imevunja rekodi ya ushindi, kupata pointi nyingi na mabao mengi msimu huu na kuwa timu ya kwanza ya Uingereza kufikia rekodi ya pointi 100 wakati Gabriel Jesus alipofunga bao la dakika za mwisho wakati wakiifunga Southampton 1-0.
Man City pia imeweka rekodi katika Ligi Kuu kwa kuwa na pointi nyingi dhidi ya timu inayofuatia ya Manchester United, ambayo ilishinda bao 1-0 dhidi ya Watford kwenye Uwanja wa Old Trafford.

No comments:

Post a Comment