Friday 25 May 2018

Liverpool, Real Madrid ni Mpambano wa Kufa Mtu

Mohamed Salah wa Liverpool.

KIEV, Ukraine
HATMA mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya yanafikia tamati kesho wakati Liverpool itakapoikabiri Real Madrid katika mchezo wa fainali utakaofanyika mjini hapa.

Ulikuwa mchezo wa Kundi B kwenye Uwanja wa Bernabeu Novemba 4 mwaka 2014. Ni mfano mkubwa wa mabadiliko ya jinsi mambo yalivyobadilika kwa Liverpool wakati mambo yakiwa vile vile kwa Real Madrid.

Timu mwenyeji itakuwa na wachezaji tisa katika kikosi cha kwanza huko Kiev leo Jumamosi, wakati tofauti na kocha wa Liverpool Jurgen Klopp kwa upande wake.

Ni taarifa kubwa kuhusu mchezo wa makundi, ambapo Liverpool ilipoteza kwa uchache kwa bao la kipindi cha kwanza la Karim Benzema, lakini dakika 90 ziliihakikishia nafasi Real Madrid.

Kipigo cha Liverpool na kocha wa wakati huo, Brendan Rodgers aliyeweka kikosi dhaifu, kiichangia kufungwa kwa timu hiyo ikiwa ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 24 katika msimu uliopita.
Cristiano Ronaldo wa Real Madrid.
 Rodgers alimpumzisha nahodha wa England Steven Gerrard pamoja na mchezaji mwenzake wa timu hiyo Raheem Sterling na Jordan Henderson, pamoja na mchezeshaji Mbrazil Philippe Coutinho.

Liverpool ilifungwa bao 1-0 na kukawa na tetesi kuwa Rodgers aliisaliti historia na utamaduni wa klabu hiyo ambayo imeshinda taji hilo mara tano na kuwaangusha maelfu wa mashabiki wa timu hiyo.

Kwa upande wa mabingwa watetezi Real Madrid, wenyewe walifika mapema kuendelea na mazoezi hapa Kiev kwa ajili ya mchezo huo wa leo Jumamosi wakati mabingwa hao mara 12 wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wakitaka kutetea taji hilo kwa mara ya tatu mfululizo.

Hatahivyo, Real Madrid wasitarajie mteremko kwa Liverpool iko vizuri na ina safu kali ya ushambuliaji, ambayo imetoa mchezaji aliyefunga mabao mengi katika Ligi Kuu ya England msimu uliomalizika.

Raphael Varane, Sergio Ramos, Marcelo, Luka Modric, Toni Kroos, Isco, Cristiano Ronaldo na Benzema wataanza katika kikosi cha kwanza. Gareth Bale atakuwa katika benchi lakini akitarajia kuingia wakati wowote.
 
Mchezaji bora wa msimu, Mohamed Salah, Roberto Firmino na Sadio Mane watakuwa katika safu ya ushambuliaji wakati wakijaribu kuishtua Real Madrid wakirejea walivyofanya mwaka 2014.

Salah, Firmino na Mane wana magoli 29 kati yao msimu huu katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na jumla wana mabao 90 wakati wakitengeneza utatu mtakatibu katika ushambuliaji huku kocha wao Klopp akiwa na matumaini ya kuibuka na ushindi leo Jumamosi.

No comments:

Post a Comment