Thursday 24 May 2018

DStv Kutangaza Kombe la Dunia Kwa Kiswahili

Wadau mbalimbali wa michezo wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface (watatu kushoto) wakipata futari jana katika hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
ZIKIWA zimebaki siku kadhaa kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia nchini Urusi, Kampuni ya Mult-Choice kupitia king’amuzi chake cha DStv, itatangaza mechi zote za Kombe la Dunia kwa lugha ya Kiswahili.
Akizungumza wakati wa hafla ya kuzindua  wa mashindano hayo, Mkuu wa Uendeshaji wa Mult’Choice Tanzania Ronald Selukindo alisema kuwa wametenga chaneli sita, ambazo zitakuwa maalum kwa Kombe la Dunia, ambalo linaanza Urusi kuanzia Juni 14 hadi Julao 15.
Alisema chaneli hizo zote zitaonekana kwa kiwango cha hali ya juu, ambacho ni cha HD, ambacho kitawawezesha wateja kuona mechi zote za Kombe la Dunia kwa picha zenye ubora wa hali ya juu.
Mwenyekiti wa zamani wa kilichokuwa Chama cha Soka Tanzania (FAT), Muhidin Ndolanga (wa pili kushoto) wakati wa kufuturu futari iliyoandaliwa na MultChoice Tanzania jana katika hoteli ya Serena.
 
“Hii ni zaidi ya ofa” alisema Ronald Shelukindo, “Sasa tunataka Watanzania waweze kupata burudani ya Kombe la Dunia 2018 kwa namna tofauti kabisa. Kwanza kwa wateja wapya wataweza kujiunga kwa Sh 79,000 tu na kupata seti ya DStv pamoja na kifurushi cha miezi miwili bure!” alisema Shelukindo.

Pia alisisitiza kuwa mbali na kutangaza kwa kugha ya Kiswahili kwa kutumia watangazaji wa michezo waliobobea wa hapa nchini pamoja na wachambuzi wake, ambao watakuwa nchini wakitangaza na kuchanbua mechi hizo kwa Kiswahili.
 

Alisema pia wateja wa DStv sasa wataweza kutazama chaneli hizo popote kupitia katika simu zao za mkononi, na tablet
Akitoa maelezo kuhusu jinsi DStv ilivyojizatiti kuwahakikishia Watanzania burudani isiyo na kifani msimu huu wa Kombe la Dunia, Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania, Alpha Mria, amebainisha kuwa DStv itaonesha michuano hiyo katika vifurushi vyake vyote,
 “Kwakeli msimu huu wa Kombe la Dunia, kila atakayekuwa na DStv atakuwa anapata kile anachostahili, kwani mechi zote zitaonekana live, kwenye HD na kwenye vifurushi vyote, huku pia zikitangazwa kwa lugha mbalimbali, ikiwemo lugha ya Kiswahili,” alisema Alpha.
Alisema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha kila mtu anapata matangazo kupitia lugha anayoitaka kama Kifarasa, Kiingereza na lugha zingine ikiwemo lugha adhimu ya Kiswahili.
 “Tumejipanga, kuwapa Watanzania burudani ya aina yake msimu huu wa Kombe la Dunia,” alisisitiza Alpha.
Katika uzinduzi huo, DStv iliwatambulisha rasmi watangazaji wa soka, ambao watakuwa wakiwaletea Watanzania matangazo ya Kiswahili, ambao ni Aboubakary Liongo, Maulid Kitenge, Ephaim Kibonde, Edo Kumwembe, Ibrahim Masoud - Maestro na Oscar Oscar.
Wakiongea baada ya kutambulishwa, watangazaji na wachambuzi hao mahiri wa soka wamesema wamejizatiti kikamilifu kuhakikisha kuwa wanawaletea matangazo na uchambuzi wa kina ili kuhakikisha kuwa kila mpenda soka anafurahia na kuyaelewa vizuri mashindano hayo.

Aidha, MultChoice ilifurisha wadau mbalimbali wa michezo jana jioni katika hoteli ya Serena kabla ya kufanyika kwa uzinduzi rasmi wa Kombe la Dunia 2018 kwa kiswahili.


No comments:

Post a Comment