Saturday 19 May 2018

Ajali ya Ndege Yaua 100 Cuba, Watatu Wanusurika


HAVANA, Cuba
ZAIDI ya watu 100 wamekufa baada ya ndege aina ya Boeing 737 kuanguka jirani na kiwanja kikubwa cha ndege cha Cuba mjini hapa, ikiwa ni ajali mbaya zaidi ya anga kuwahi kutokea katika miongo kadhaa.

Wanawake watatu waliokolewa wakiwa hai kutoka katika mabaki ya ndege hiyo, lakini wakiwa katika hali mbaya sana.

Ndege hiyo, ambayo inakaribia umri wa miaka 40 tangu itengenezwe, ilikuwa imepakia abiria 104 na wafanyakazi sita.

Mamlaka ya Cuba imeanzisha uchunguzi, huku ikitangaza siku mbili za maombolezo kutokana na ajali hiyo.

Ndege hiyo aina ya Boeing 737-201 iliyokuwa ikifanya safari za ndani, ilianguka majira ya saa 10:08 jioni juzi, muda mfupi baada ya kupaa kutoka katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha José Martí  jijini Havana wakati ikienda kwenye Kiwanja cha Frank Pais huko Holguin, mashariki ya kisiwa hiki.
 
Wafanyakazi wote wa ndege hiyo walikuwa ni raia wa Mexico, huku abiria wengi wakiwa ni raia wa Cuba, huku miongoni mwao walikuwa abiria watano wakigeni.

"Kuna ajali mbaya ya anga imetokea. Habari hazifurahishi na inaelekea kuna idadi kubwa ya abiria wamekufa, “alisema Rais wa Cuba, Miguel Diaz-Canel alipotembelea eneo la tukio, ndege hiyo ilipoangukia.

Nini sababu za ajali?

Taarifa zilisema kuwa ni mapema mno kusema sababu za ajali hiyo, lakini mashuhuda waliokuwa chini walielezea kuwa waliiona ndege hiyo ikilipuka kabla ya kuanguka msituni jirani na kiwanja kikubwa cha ndege cha Havana.

"Niiona ndege hiti ikiruka, “alisema mfanyakazi mmoja wa duka kubwa Jose Luis aliliambia Shirika la Habari la AFP. “Mara, iligeuka, na kuanguka chini. Wote tulishangaa.”

"Tulisikia mlipuko na badae tuliona moshi mkubwa ukieenda juu, “alisem aGilberto Menendez, ambaye anaendesha mgahawa mmoja jirani na eneo lililotokea ajali hiyo.

Idara ya usafiri ya Mexico ilisema katika mtandao wake kuwa “wakati ikipaa (ndege hiyo) ilipata matatizo na kurudi chini.”

Kampuni ya Boeing ilisema kuwa iko tayari kupeleka timu ya mafundi Cuba kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kina kujua tatizo lililoisibu ndege hiyo hadi kuanguka.

Watu Walionusurika

Waru wanne walinusurika katika jail hiyo lakini mmoja alikufa mara baada ya kufikishwa hospitalini, alisema mkurugenzi wa hospitali ya Calixto Garcia iliyopo Havana, Carlos Alberto Martinez.

Watui hao watatu walionusurika wote ni wanawake, kwa mujibu wa gazeti la Chama cha Kikomunisti  la Granma: mmoja akiwa na umri kati ya miaka 18 na 25, wakati mwingine mwenye umri wa miaka 13 wakati watatu ana miaka 39.

"Yuko hai lakini ameungua vibaya, “alisema ndugu ya mwanamke huyo katika hospitali hiyo.

Nchi zote, Argentina na Mexico zilithibitisha kuwa wananchi wa mataifa yao ni miongoni mwa waliokufa katika ajali hiyo.

Tunachijua Kuhusu Ndege
Ndege hiyo ilitolewa na kampuni ya Mexico ya Aerolines Damojh kwa shirika la ndege la serikali la Cuba la Cuban de Aviación.

Mamlaka ya Mexico ilisema kuwa ndege hiyo ilitengenezwa mwaka 1979 na ilikaguliwa Novemba mwaka jana. Mexico imesema kuwa imetupa wataalam wawili wa mabo ya anga kusaidia katika uchunguzi huo.

Aerolineas Damojh, ambayo pia inajulikana kama Global Air, ina ndege tatu ambazo zinafanya kazi.

Ajali Zingine za Ndege

Kwa mujibu wa tafiti, mwaka jana ndege ya biashara ambayo ilikuwa ikisafiri bila abiria, ilianguka. Lakini mwaka huu kumekuwa na ajali kibao mbaya za ndege.

Mwezi uliopita, ndege ya jeshi ilianguka na kuua zaidi ya watu 250. Februari , ndege ya Saratov Airlines ilianguka karibu na Moscow, iliua watu 71 mwezi Machi, ndege ya Marekani ya Bangla Airlines ilianguka Kathmandu, Nepal; iliua watu 51.

Ajali nyingine mbaya ya ndege ilitokea mwaka 1989, wakati ndege ya abiria  iliyotengenezwa nchini Urusi aina ya Ilyushin-62M ilianguka jirani na jiji la Havana na kuua abiria wote 126 waliouwemo ndani ya ndege hiyo na wengine 24 waliokuwa ardhini.

No comments:

Post a Comment