Monday 14 May 2018

Swansea City Yashuka Daraja Baada Misimu Saba


LONDON, England
TIMU ya Swansea City imeteremka daraja baada ya misimu saba kucheza Ligi Kuu ya England, baada ya kupokea kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Stoke City, ambayo tayari ilishatangulia katika Ligi Daraja la Kwamza.

Swansea City imemaliza ligi hiyo inayoshirikisha jumla ya klabu 20 ikiwa katika nafasi ya 18 baada ya kujikusanyia jumla ya pointi 33 ikiwa pointi sawa na Stoke City iliyopo katika nafasi ya 19 huku West Bromwich Albion ikishika mkia ikiwa na pointi 31.

Klabu hiyo ya Welsh ilihitaji mabo 10 ili iweze kubadili matokeo na kuiporomosha Southampton, kitu ambacho haikutokea na kushangaza yenyewe ndio imeporomoka baada ya misimu saba ya kucheza ligi hiyo.

Lakini hadi mapumziko, Swansea City, ambayo haijashinda mchezo wowote ugenini katika mechi 13 zilizopita, iliongoza kwa bao la Msenegal Badou Ndiaye na baadae Peter Crouch. Xherdan Shaqiri walifunga kwa Stoke huku pia ikikosa penalti.

Kocha Mreno wa Swansea City, Carlos Carvalhal ana nafasi kubwa ya kuondoka katika klabu hiyo, miezi mitano tangu aanze kuifundisha.

"Jana nilizungumza na mmiliki, jana Jumatatu tulitarajia kuzungumza tena, “alisema.
"Mimi mwenyewe nitafikiria kuhusu Swansea na nitazungumza na famnilia yangu. Baada ya hapo nitatoa uamuzi sahihi kuhusu hatma yangu.

"Najua Ligi Daraja la Kwanza na tulifikia hatua ya mchujo mara mbili. Hiyo sio kawaida timu kucheza mchujo mara mbili mfululizo.”

Kocha wa Stoke City Paul Lambert naye pia muda wake wa kuifundisha timu hiyo haukutosha kubadili mambo baada ya kuanza kuifundisha timu hiyo Januari.
"Kuna mambo hayako vizuri, hilo halina wasiwasi, “alisema.

No comments:

Post a Comment