Monday 31 July 2017

MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUHUSU WAGENI 16 WALIOlNGIA NCHINI KUPITIA JENGO LA WATU MASHUHURI (VIP LOUNGE)

Tarehe 31/07/2017 ehombo kimoja eha habari kilitoa taarifa za upotoshaji kwamba wageni 16 wenye uraia wa Lebanon, Pakistani na Somalia walinaswa katika Kiwanja eha Ndege eha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) baada ya kupita Jengo la Watu Mashuhuri (VIP).

Taarifa sahihi za suala hili ni kwamba Tarehe 30107/2017 abiria wanne (4) Raia wa Taifa la Pakistan waliwasili kwenye Kiwanja eha Ndege eha Kimataifa eha Julius Nyerere (JNlA) na kupita Jengo la Watu Mashuhuri (VIP Lounge) ambapo nyaraka zao za safari zilikaguliwa na Maafisa wa Uhamiaji na baadae kuruhusiwa kuingia nehini baada ya kujiridhisha kuwa ni halali.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Salim Msangi.
Abiria hao walikuwa na kibali kinaehowaruhusu kutumia ukumbi wa watu mashuhuri (VIP) kiliehotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.

Utaratibu uliopo katika matumizi ya Ukumbi wa watu Mashuhuri (VIP Lounge) JNIA ni kwamba wageni wote toka nje ya nehi wanaohitaji kutumia ukumbi huo wanalazirnika kuomba kibali Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa na Wizara husika inapojiridhisha na vigezo vya waombaji,hutoa vibali hivyo.

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) inatoa wito kwa vyombo vya habari nehini kuandika habari kwa weledi na kuhusisha pande zote zinazohusishwa katika taarifa zao mbalimbali, iii kuepuka mkanganyiko na upotoshaji kwa jamii kwa jambo husika.

TAA ipo tayari kutoa ushirikiano kwa chombo chochote cha habari kinachowasiliana nacho kutaka ufafanuzi wajambo fulani, ili waweze kuandika kwa umakini na ufasaha zaidi.

IMETOLEWA NA:
KAIMU MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA (TAA) \--=1; .BW. SALIM MSANGI

No comments:

Post a Comment