Monday 3 July 2017

Serikali yavipa neno zito vyama vya michezo

Naibu waziri wa Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo, Anastazia Wambura (katikati waliokaa) akiwa pamoja na washiriki na wakufunzi wa mafunzo ya ualimu wa Level 1 wa wachezaji wenye  umri aw miaka 16 iliyoanza leo katika Kituo cha Michezo cha Filbert Bayi Nkuza Kibaha.
Na Mwandishi Wetu, kibaha
SERIKALI imesema Tanzania inatakiwa kuanza mapema maandalizi ili kupata medali katika mashindano mbalimbali yajayo ya kimataifa.

Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Harrson Mwakyembe wakati akifungua mafunzo ya siku 13 ya makocha wa riadha ya hatua ya kwanza ya wachezaji wenye umri chini ya miaka 16 katika Kituo cha Michezo cha Filbert Bayi Mkuza, Kibaha mkoani Pwani.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura.
 Akizungumza kwa niaba ya Mwakyembe, Naibu Waziri wa wizara hiyo, Anastazia Wambura alisema kuwa, vyama vya michezo lazima kuanza mapema maandalizi ya kushiriki mashindano ya kimataifa ili kuiwezesha nchi kupata medali katika michezo ijayo.

Tanzania inatarajia kushiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Gold Coast, Australia 2018, ile ya Mataifa ya Afrika 2019 na Olimpiki itakayofanyika Tokyo, Japan 2020.
Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) akizunguza wakati wa mafunzo hayo.
Waziri alisema kuwa taifa lina vipaji vingi, lakini tatizo kubwa ni ufinyu wa maandalizii ya maana na kuhitaji makocha wenye uwezo mkubwa wenye uzoefu wa kimataifa ili kuwaandaa vizuri kisayansi wachezaji kwa ajili ya mashindano hayo.

Dk Mwakyembe alisema kuwa Tanzania inaweza kufanya maajabu katika mashindano ya kimataifa kutokana na vipaji vilivyopo katika michezo mbalimbali kama wachezaji wataandaliwa vizuri na mapema.
Makamu wa Rais wa TOC, Henry Tandau (kulia) na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura. Kulia kwa Waziri ni Makamu wa Pili wa Rais Riadha Tanzania (RT), Dk Hamad Ndee. 
 “Tunatakiwa kuwaandaa vizuri wanariadha wetu kwa ajili ya mashindano ya kimataifa kutoka kwa makocha wenye uzoefu mkubwa ambao watauwezesha kuupeleka mbele mchezo wetu huu wa riadha, “ alisema wakati akizungumza na washiriki kutoka zaidi ya mikoa 10 ya Tanzania Bara na Zanzibar.

"Tuna mashindano makubwa mbele yetu, kama Jumuiya ya Madola 2018 Australia, Michezo ya Afrika 2019 Guinea ya Ikweta na ile ya Olimpiki mwaka 2020. “ alisema.

"Sasa tunatakiwa kuangalia mbele maandalizi ili kuweza kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ya kimataifa, “alisema.
Mwakyembe alisema alibaini vipaji katika mashindano ya vijana ya wachezaji wenye umri wa chini ya miaka 18 ya riadha iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi karibuni wakati wanariadha chipukizi walipoonesha  uwezo wa hali ya juu.

Pia aliitaka Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) kuratibu vizuri kozi hiyo kwa kushirikiana na vyama vya michezo vya Tanzania (RT) na kile cha Zanzibar (ZAAA) chini ya udhamini wa Mshikamano wa Olimpiki ((OS).

Mafunzo hayo yanashirikisha washiriki kutoka mikoa ya Mbeya, Singida, Mara, Kagera, Dar es Salaam, Zanzibar, Mwanza,Dodoma, Ruvuma, Arusha, Pwani, Simiyu, Iringa, Kilimanjaro, Njombe na Shinyanga.
Akizunumza mapewa mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo kutoka Uganda, Charles Mukiibi  alisema mafunzo hayo yanaleng katika kutoa ujuzi wa kufundisha watoto wenye umri chini ya miaka 16 na chini yake, wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa shule za msingi, ambao wanalenga kuwa mabingwa wa baadae.

Makamu wa Rais wa Riadha Tanzania (RT), Dk Hamad Ndee alisema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka kwani yatasaidia kuongeza idadi ya makocha wa mchezo huo hapa nchini.
Aliwataka washiriki kutumia mafunzo hayo vizuri ili kuja kuwa makocha wazuri wa vijana.

"Tunaishukuru TOC kwa jitihada kubwa walizofanya hadi kutupatia mafunzo haya, ambayo yatatusaidia kuuendeleza mchezo huu hapa nchini, “alisema Katibu Mkuu wa ZAAA, Suleiman Ame wakati akitoa salama za shukrani kwa niaba ya washiriki wote.
Alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia mikoa kutoa wanariadha wengi chikupukizi ambao watafanya vizuri siku za usoni.

Naye katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi alisema kozi hiyo imeratbiwa na RT na ZAAA pamoja na TOC.

Bayi,ambaye ni gwiji wa zamani wa riadha Tanzania alisema kuwa vyana vya riadha vya mikoa haviko hai kutokana na ukosefu wa wanariadha chipukizi, ambao vipaji vyao haviendelezwi.
Alisema tayari TOC imeshatoa kozi 19 kwa viongozi wa vyama vya michezo vya kitaifa na makocha  katika harakati za kuendeleza michezo nchini.

Alisema ni jukumu la vyama vya michezo kuhakikisha mafunzo hayo yaliayoanza mwaka 2005, yatoa matunda.

Alisema kuwa TOC imekuwa ikifanya kazi bila kuchoka kuhakikisha Tanzania inatoa wakimbiaji watakaofanya vizuri katika mashindano mbalimbali.
Alisema kuwa Tanzania  inahitaji wanariadha chipukizi ikiwa nchi iliyopo katika 10 bora zilizoshiriki katika Michezo ya Olimpiki iliyofanyika Rio de Janeiro 2016.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Makamu wa Rais wa TOC, Henry Tandau alisema ufinyu wa program za maendeleo kwa vyama vya michezo, masoko na udhamini ni miongoni mwa viti vinavyorudisha nyuma maendeleo ya michezo hapa nchini.


Vyama vya michezo vinatakiwa kuwa na program za uhakika na kuelekeza maandalizi yao katika mashindano makubwa badala ya kusubiri muda umekwisha ndio wafanye maandalizi ya zima moto.

No comments:

Post a Comment